Jumapili, 31 Machi 2019

NDALICHAKO AZINDUA MAKTABA MTANDAO TAASISI YA ELIMU TANZANIA -TET


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amezindua Maktaba Mtandao ya Taasidi ya Elimu Tanzania (TET).

Akizindua Maktaba hiyo jijini Dar es salaam Waziri Ndalichako amesema itasaidia kupunguza changamoto iliyopo ya usambazaji wa vitabu kwani mara nyingi vimekuwa vikichelewa kufika katika shule kutokana na ugumu wa miundombinu ya usafirishaji na kuleta usumbufu katika mchakato wa ujifunzaji na ufundishaji.

Amesema Serikali imeiona changamoto hiyo na kuanzisha Maktaba Mtandao kama  moja ya njia ya kurahisisha upatikanaji wa machapisho ya Kiada, Ziada, Mitaala Mhtasari, Kiongozi cha Mwalimu, Miongozo mbalimbali na Moduli za Kufundishia na kujifunzia kwa wanafunzi walimu na watumiaji wengine.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Joyce Ndalichako akizinduz Maktaba Mtandao ya Taasisi ya Elimu Tanzania katika uzinduzi wa Maktaba hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam
“Kumekuwa na lawama katika suala la usambazaji wa vitabu kwani havifiki kwa wakati, kawaida mwanafunzi anapaswa kukuta vitabu shuleni lakini hali ilivyo sasa vitabu vinamkuta mwanafunzi shuleni hii si sawa, hivyo kuwepo kwa Maktaba Mtandao itasaidia katika kupatikana kwa vitabu mapema na kurahisisha mchakato wa kujifunza" amesisitiza Waziri Ndalichako.
Wakati huo huo Ndalichako ameiagiza Bodi ya Taasisi ya Elimu Tanzania(TET) kuhakikisha inasimamia uandaaji wa machapisho ya mitaala, vitabu na machapisho mengine  ili yawe na ubora.
Ameeleza kuwa pamoja na Bodi hiyo kufanya kazi nzuri ya kusimamia na kuhakikisha vitabu vinavyochapishwa sasa vinakuwa na ubora lakini bado inapaswa kongeza umakini kwa sababu suala la uandaaji wa vitabu ni endelevu.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Joyce Ndalichako akiangalia maonesho ya vitabu vinavyoandaliwa na Taasisi ya Elimu Tanzania wakati wa uzinduzi wa  Maktaba Mtandao jijini Dar es Salaam

Ndalichako amesisitiza kuwa TET ni moyo wa Elimu nchini kwa kuwa ndio inaandaa mitaala, vitabu, miongozo ya shule za msingi na sekondari pamoja na machapisho mbalimbali ya Elimu, hivyo kukiwa na kasoro katika mchapisho hayo watoto wa Kitanzania watakuwa wamefundishwa vitu ambavyo si sahihi na serikali haitavumilia hilo.

Awali Mkurgenzi wa Taasisi ya Elimu Tanzania Dkt Aneth Komba alimweleza Waziri wa Elimu kuwa lengo la kuanzishwa maktaba mtandao hiyo kurahisisha usambazaji wa machapisho ya Taasisi hiyo katika shule za Serikali, Binafsi na kwa wadau wengine wa Elimu
Dkt Komba amesema  Maktaba Mtandao iliyozinduliwa inajumuisha vitabu mbalimbali vya kiada kuanzia ngazi ya Elimu ya awali, msingi na sekondari (kidato cha kwanza mpaka sita)  vinavyochapishwa na taasisi hiyo. Pia vitakuwepo vitabu vya  ziada kutoka Tanzania na Nchi nyingine.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Joyce Ndalichako akicheza na kufurahi na wanafunzi wa shule ya Fountain Gate wakati wa uzinduzi wa  Maktaba Mtandao ya Taasisi ya Elimu Tanzania katika uzinduzi wa Maktaba hiy iliyofanyika jijini Dar es Salaam


Maoni 4 :

  1. Tunavipataje hivyo vitabu vya mtandaoni kwa wale wenye watoto ambao wako kijijini na hakuna huduma zinazoweza kupata vitabu hivi kama vile...internet,umeme,computer nk? Au huduma hii imelega kusaidia watoto wenu walio na uwezo wa kupata miundombinu hiyo? Je mtoto wa mwananchi myonge mnamsaidiaje ili aweze hata kwenda mjini na kuprint vitabu hivi ili ajisomee??

    JibuFuta
  2. Nashauri kipindi hiki serikari ingegaramia kumpa kila mtoto vitabu vya masomo ili ajisomee hasa watoto ambao hawana computer nyumbani ili wajisomee hya ya mtandao yatanufaisha wachache tu.

    JibuFuta
  3. Kuwa na kipindi maalum kwenye redio ya taifa TBC

    JibuFuta
  4. Tunaomba link ya kuvipata hivyo vitabu vya watoto wa shule za msingi.

    JibuFuta