Alhamisi, 23 Aprili 2020

NAIBU WAZIRI OLE NASHA AWAPONGEZA WABUNGE KUJENGA SHULE YA WASICHANA


Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Ave Maria Semakafu wakikagua ujenzi wa miundombinu ya shule ya sekondari maalum ya wasichana inayojengwa na Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyopo Chamwino, Dodoma.
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha amefanya ziara kukagua maendeleo ya ujenzi wa shule maalum ya wasichana inayojengwa na wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Kata ya Kikombo wilayani Chamwino Jijini Dodoma

Kiongozi huyo amesema lengo la ziara hiyo pamoja na mambo mengine ni kuona maeneo ambayo Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia itaweza kuchangia ili kukamilisha ujenzi wa shule hiyo katika muda uliopangwa.
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha akikagua ujenzi wa miundombinu mipya ya shule ya sekondari maalum ya wasichana wa kidato cha tano inayojengwa na Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyopo Chamwino, Dodoma. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Ave Maria Semakafu.
Naibu waziri Ole Nasha amewapongeza wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuona umuhimu wa kujenga shule ya wasichana kwani kumuelimisha mtoto wa kike ni sawa na kuelimisha jamii nzima.

Shule ya Wasichana ya Bunge ilianza kujengwa Januari 2020 itakamilika Juni mwaka huu na inatarajiwa  kuchukua wanafunzi wa kidato cha tano. 

Katika ziara hiyo Naibu waziri Ole Nasha aliambatana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Ave Maria Semakafu.



Muonekano wa baadhi ya majengo ya shule ya sekondari maalum ya wasichana inayojengwa na Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyopo Chamwino, Dodoma.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni