Jumatano, 1 Mei 2019

WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA YAPONGEZWA KWA KUBORESHA CHUO CHA UALIMU MPUGUSO


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Joseph Magufuli amefurahishwa na mradi wa ujenzi na ukarabati wa Chuo cha Ualimu Mpuguso kilichopo katika Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya na ameipongeza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa mradi huo.

Rais Magufuli amesema hayo wakati wa hafla ya uwekaji jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa majengo mapya na ukarabati katika Chuo hicho kwa lengo la kuboresha na kuongeza miundo mbinu ili kuongeza nafasi na kuweka mazingira bora ya ufundishaji na ujifunzaji.

“Niwapongeze Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kukiboresha Chuo hiki ambacho ni cha zamani kilianza mwaka 1926 ikiwa ni shule ya awali hadi mwaka 1975 kilipobadilishwa kuwa Chuo cha Ualimu na sasa kuna wanafunzi zaidi ya 900,” amesema Rais Magufuli.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akivuta utepe pamoja na viongozi wengine kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi wa Majengo mapya ya Chuo cha Ualimu Mpuguso Rungwe mkoani Mbeya. 

Katika hatua nyingine akizungumza na wananchi baada ya uwekaji jiwe la msingi amesema Serikali yake imeamua kuboresha Vyuo vya Ualimu ili viweze kuandaa walimu bora na kusisitiza kuwa ajira za waalimu watumishi wengine kwenye sekta ya elimu zinaendelea kutolewa ambapo zaidi ya watumishi 19,000 wenye sifa wameajiriwa mwaka huu,  huku akiwataka waalimu wanafunzi kuongeza juhudi katika masomo na kutembea kifua mbele kwani Serikali iko pamoja.

Rais Magufuli pia amewataka Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, pamoja na Mkandarasi anaejenga Chuo hicho kuhakikisha kazi inakamilika kwa wakati na kwa ubora unaolingana na thamani ya fedha ya mradi. Aidha ameagiza Barabara inayoingia katika Chuo hicho kurekebishwa na baadae kutengewa fedha ili iweze kujengwa kwa kiwango cha lami.

Awali akitoa taarifa ya mradi wa Mpuguso, Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leornard Akwilapo amesema unagharimu shilingi Bilioni 9.6 na unahusisha ujenzi wa vyumba vya madarasa 16, maktaba, maabara 2 za sayansi, kumbi za mihadhara 2, bwalo la chakula, mabweni 2 ya wanafunzi 154 kila moja na nyumba za walimu zinazochukua familia 13.  Amesema mradi huo pia unahusisha ukarabati wa nyumba 4 za walimu, mabweni 2 , vyoo na mabafu7.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wananchi wa Mpuguso Rungwe mkoani Mbeya mara baada ya kuweka jiwe la msingi msingi ujenzi wa Majengo mapya ya Chuo cha Ualimu Mpuguso.


Mradi wa Ukarabati na ujenzi wa majengo mapya katika Vyuo vya Ualimu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania na Canada, ambapo unahusisha vyuo vya ualimu 4 kikiwemo Mpuguso.  Vingine ni Kitangali Mtwara, Shinyanga na Ndala kilichopo Tabora. Kwa ujumla Mradi huu utagharimu shilingi Bilioni 36.4

Nae Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (Mb) amepongeza wana Mpuguso kwa  kupata mradi huo mkubwa na kuwaasa kuhahakikisha wanatumia vizuri majengo hayo na kuyatunza.

Hafla hiyo ilihudhuriwa mamia ya wananchi wa Rungwe na viongozi akiwemo Mhe. Dkt. Tulia Akson Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Tanzania, Mhe. Suleiman Jafo(Mb) Waziri wa TAMISEMI, Mhe. Japhet Hasunga(Mb) Waziri wa Kilimo, Mhe Joseph Kakunda(Mb) Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Mary Mwanjelwa(Mb) Naibu Waziri Utumishi na Mh Elias Kwandikwa(Mb) Naibu Waziri wa Ujenzi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiimba pamoja na wananchi waliokusanyika katika viwanja vya Chuo cha Ualimu Mpuguso mara baada ya kuwasili chuoni hapo.

Ijumaa, 26 Aprili 2019

WAZIRI NDALICHAKO AIPONGEZA CHINA KWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA TANZANIA


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako ameipongeza Jamhuri ya Watu wa China kwa kuimarisha ushirikiano  na  Tanzania hususan katika sekta za Elimu, Biashara na Ujenzi wa miundombinu.

Waziri Ndalichako ametoa pongezi hizo wakati wa sherehe za kuadhimisha miaka 55 ya uhusiano wa Kidiplomasia kati ya Tanzania na China ambapo amesema kuwa mahusiano kati ya nchi hizo mbili ni ya muda mrefu.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akizungumza katika sherehe za kuadhimisha miaka 55 ya uhusiano wa Kidiplomasia kati ya Jamhuri ya Watu wa China na Jamhri ya Muungano wa Tanzania.

Aidha, Prof. Ndalichako amesema mchango wa nchi hiyo kwenye maendeleo ya Tanzania ni dhahiri akitolea mfano  wa ujenzi wa Reli ya TAZARA pamoja na ujenzi wa viwanda mbalimbali vya nguo nchini.

Prof. Ndalichako amesema pia China imeendelea kushirikiana na Tanzania kwenye Sekta ya Afya kwa kubadilishana uzoefu.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akifuatilia hotuba iliyokuwa ikitolewa na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China, Wag Ke (Hayupo pichani) katika sherehe za kuadhimisha miaka 55 ya uhusiano wa Kidiplomasia kati ya China na Tanzania.

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo  Pinda, Viongozi mbalimbali wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb), Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia Bw. Caesar Waitara, na viongozi mbalimbali kutoka Taasisi  za umma na binafsi nchini. 

Alhamisi, 25 Aprili 2019


UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY
SCHOLARSHIP TENABLE IN THE GOVERNMENT OF PAKISTAN
2019-2020
Call for Application
The General Public is hereby informed that, the Government of Pakistan has offered scholarships opportunity to Tanzanian to study Master’s degree programme in the Public Universities.  Eligible candidates may apply in field of Social Sciences, Gender Studies, Arts & Humanities, Management and Business Education, Agriculture and Veterinary Sciences, and Natural Sciences/Physical Sciences.

For further information, Procedure for application, Fields of study, Financial breakdown, Eligibility criteria, Required documents, Universities and Admission procedure please visit the following link:http://www.hec.gov.pk/english/scholarshipsgrants/ARL-FS/CWLDC/Pages/default.aspx
The application should be completed no later than May 15th, 2019.
Issued by:
Permanent Secretary,
Ministry of Education, Science and Technology,
University of Dodoma,
College of Business and Law,
Block 10,
P .O. Box 10,
40479 Dodoma.

UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY


  STUDY OPPORTUNITY OFFERED BY THE ORGANIZATION FOR WOMEN IN SCIENCE FOR THE DEVELOPING WORLD (OWSD-EARLY CAREER FELLOWSHIP) 2019/2020

Call for Application
The General Public is hereby informed that, Organization for Women in Science for the Developing World (OWSD) has offered scholarships opportunity to Tanzanian women. The OWSD Early Career fellowship is a prestigious award of up to USD 50,000 offered to women who have completed their PhDs in Science, Technology, Engineering and Mathematics (STEM) subjects and are employed at an academic or scientific research institution in one of the listed Science and Technology Lagging Countries (STLCs). The OWSD Early Career fellows will be supported to establish an environment at their institution where they can maintain an international standard of research and attract scholars from all over the world to collaborate.

Mode of Application

Note: The official language for the application is English; however, all information about the programme is also available in French at: https://bit.ly/2IKPfRZ.

Submission
Online application must be submitted not later than 30th April, 2019.

Issued by:
Permanent Secretary,
Ministry of Education, Science and Technology,
University of Dodoma,
College of Business and Law,
Block 10,
P .O. Box 10,
40479 DODOMA.