Ijumaa, 6 Machi 2020

MAKTABA MPYA YAZINDULIWA CHUO CHA UALIMU KOROGWE

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa  Machi 5, 2020 amezindua maktaba mpya ya  Chuo cha Ualimu Korogwe kilichopo Mkoani Tanga.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akikata Utepe kuashiria uzinduzi wa Maktaba mpya ya Chuo cha Ualimu Korogwe, Tanga kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mh Martin Shigela, Mbunge wa Korogwe Mjini Mhe. Mary Chatanda na Kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Elimu , Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo
 Akizungumza na baadhi ya walimu tarajali na wanafunzi aliowakuta katika maktaba hiyo mara baada ya kuizindua Waziri Mkuu amewataka wanafunzi hao kuitumia vyema maktaba hiyo kwa lengo la kujipatia maarifa na kuongeza uwezo katika taaluma.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa Majaliwa akipata maelezo toka kwa mtaalamu wa Tehama wa Chuo cha Ualimu Korogwe baada ya kuzindua Makataba ya Chuo hicho
Naye Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi  na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo akimkaribisha Waziri Mkuu amesema
Serikali imetoa zaidi ya shilingi milioni 338 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa maktaba hiyo ambayo ujenzi wake ukianza kwa Micjango ya Wananchi wa Korogwe.

Katibu Mkuu huyo amesema Serikali ya Awamu ya Tano iliamua kutoa kiasi hicho cha fedha ili kuunga mkono juhudi za wananchi ambao walichanga shilingi milioni 1.9 kwa ajili ya kuanza ujenzi huo.
Chumba cha kompyuta katika Maktaba mpya ya Chuo cha Ualimu Korogwe
"Wananchi wa Korogwe waliona umuhimu wa chuo hiki kuwa na maktaba na wakaanza kuchanga fedha na kuanza ujenzi" amesema  Dkt. Akwilapo.

Mmoja wa walimu tarajali  katika Chuo cha Ualimu Korogwe Emanuela Bombo ameishukuru Serikali kwa kuwekeza kwenye ujenzi wa maktaba hiyo kwani itasaidia katika ujifunzaji.
Muonekano wa moja ya  Eneo la kujisomea katika Maktaba mpya ya Chuo cha Ualimu Korogwe
Maktaba hiyo ina vifaa vya kisasa pamoja zikiwemo kompyuta ambazo zinawezesha matumizi  maktaba mtandao na kwamba Maktana itatumiwa na walimu tarajali zaidi ya 1000 ambao wanasoma masomo ya Sayansi, Hisabati na TEHAMA na pia wanafunzi wa shule za Msingi na Sekondari wa wilaya ya Korogwe.


PUBLIC NOTES


Ijumaa, 14 Februari 2020

UKWELI KUHUSU VYUO VYA MAENDELEO YA WANANCHI (FDCs)

WAZIRI NDALICHAKO ATAKA USIMAMIZI THABITI WA MIRADI YA ELIMU

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako ametoa rai kwa watendaji wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kusimamia vizuri fedha za  miradi ya Elimu inayotelekezwa katika maeneo yao ili  ikamilike kwa wakati na ubora.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akizungumza wakati wa uzinduzi wa Jengo la  Utawala la Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam, Jijini Dar es Salaam
Waziri Ndalichako ametoa rai hiyo Jijini Dar es Salaam wakati akizinduzia Jengo la Utawala la Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) lililokarabatiwa na kuongeza ukubwa ambapo amesema Serikali imekuwa ikitoa fedha nyingi za Miradi lakini haikamiliki kutokana na usimamizi mbovu hivyo kutaka watendaji hao kusimamia miradi ipasavyo.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akizindua Jengo la Utawala la Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam, Jijini Dar es Salaam
Amesema Serikali ya Awamu ya Tano imefanya kazi kubwa sana katika kuboresha mazingira ya utoaji elimu  na kwamba kukamilika kwa mradi wa upanuzi wa Jengo la Utawala la Chuo Kishiriki cha DUCE ni sehemu tu ya mambo mengi ambayo Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na serikali yake imefanya.
Baadhi ya Wanajumuiya ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako wakati wa uzinduzi wa Jengo la Utawala la Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam, Jijini Dar es Salaam
Profesa Ndalichako aliongeza kuwa wakati Serikali ikiendelea na maboresho hayo, taasisi za elimu ya juu zinatakiwa kuendelea  kutekeleza wajibu wao ipasavyo ambao  ni kutoa taaluma, kufanya tafiti pamoja na kutoa huduma na ushauri kwa jamii.

“Vyuo Vikuu vimekuwa vikijikita katika utoaji wa taaluma wakati mwingine vinakuwa vikisahau jukumu la kufanya tafiti na ndio maana tunaona idadi ya machapisho imekuwa ikipungua mwaka hadi mwaka. Niwaambie tunapokuwa tunafanyiwa tathmini ya upangaji wa madaraja ya vyuo, sehemu ambayo mara nyingi imekuwa ikituangusha ni sehemu ya tafiti, kwa hiyo nitumie nafasi hii kuzikumbusha Taasisi za elimu ya juu kuendelea kufanya tafiti na tafiti zenyewe ziwe ni zile zinazotoa mchango moja kwa moja katika maendeleo ya nchi,” amesema Ndalichako.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Joyce Ndalichako akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanajumuiya wa Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam mara baada ya  kuzindua Jengo la utawala la chuo hicho,  jijini Dar es Salaam
Katika hatua nyingine Profesa Ndalichako ametoa wito kwa Vyuo vya Elimu ya Juu nchini kutumia vema mapato yao ya ndani yanayotokana na huduma wanazotoa  kama za ushauri na tafiti kwa maendeleo ya Vyuo ikiwa ni pamoja na  kutenga sehemu ya Mapato hayo ndani kugharamia masomo ya watumishi.

“Nakipongeza Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kuweza kutumia fedha kutoka kwenye mapato  ya ndani kutoa ufadhili wa masomo kwa watanzania wenye ufaulu wa kiwango cha Juu. Huu ni mchango mkubwa kwa Taifa letu kwani unatoa fursa kwa watanzania ambao wamefaulu vizuri lakini kutokana na sababu mbalimbali wasingeweza kunufaika na mikopo itolewayo na Bodi ya Mikopo,” alisema Waziri Ndalichako.
 
Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Chuo Kishiriki cha Dar es Salaam ambae pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Usimamizi ya DUCE Profesa William Anangisye amemuahidi Waziri Ndalichako kuendelea kusimamia vizuri matumizi ya fedha za Miradi ikiwa ni pamoja na kuhakikisha jengo lililozinduliwa leo linatumika kwa malengo yaliyokusudiwa na kuwa chachu ya maendeleo ya Chuo hicho.

“Mhe. Waziri nakuahidi kuwa majengo haya yatatunzwa vizuri na kutoa mchango mkubwa katika utekelezaji wa majukumu ya chuo,” amesema Prof. Anangisye.

Naye Kaimu Rasi wa Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE), Prof. Stephen Maluka ameishukuru Serikali kwa namna inavyoendelea kuboresha mazingira ya utoaji elimu kwa Taasisi za elimu ya Juu ambapo amesema katika Chuo hicho upanuzi wa Jengo la utawala umeondoa changamoto iliyokuwepo ya ukosefu wa ofisi za watumishi huku akiiomba Serikali kuwapatia fedha kwa ajili ya kusomesha wataalamu wao.