Jumatano, 16 Julai 2014

Waziri Mhagama akagua utekelezaji wa STHEP

Naibu  Waziri  wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi amefanya  ziara  ya kukagua utekelezaji wa Mradi wa Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu (Science, Technology and Higher Education Project - STHEP) katika  Chuo Kikuu  Huria  cha Tanzania (OUT) na Chuo  Kikuu Kishiriki cha  Elimu Dar es salaam (DUCE) ambapo amejionea mafanikio makubwa yaliyopatikana kutokana na utekelezaji wa Mradi huo.

Mafanikio hayo ni pamoja na majengo mbalimbali yaliyojengwa, vifaa vya kufundishia na kujifunzia, magari yaliyonunuliwa na Wahadhiri waliosomeshwa katika ngazi ya Shahada ya Uzamili na Uzamivu kupitia mradi huo.

“Kutokana  na kukamilika  kwa Mradi huo  katika awamu ya kwanza, Watanzania  wategemee  mabadiliko  makubwa  katika  sekta ya  Elimu  na kutoa  ubora  wa  Elimu  na  sasa tunakamilisha taratibu za kuanza  kwa awamu ya  pili  ya mradi huo  ambapo pia  tutawasomesha  walimu,” alisema Mhe. Mhagama.





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni