Jumamosi, 17 Juni 2017

MAADHIMISHO YA KILELE CHA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA.

Mkurugenzi wa Elimu ya Juu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Sylivia Temu amewataka Wazazi, walezi na walimu  kuwalea watoto  katika misingi ambayo itawafanya wawe na maadili mema ili waje kuwa viongozi, na  wazazi bora katika maisha yao ya baadae.

Profesa Temu amesema hayo hii leo katika maadhimisho ya kilele cha siku ya mtotot wa Afrika ambayo yamefanyika kwenye kijiji cha Humekwa, Wilayani Chamwino mkoani Dodoma.

Profesa Temu amesewasihi Watoto kupenda kusoma na kuacha kujiingiza kwenye makundi ya matumizi ya  dawa za kulevya, na badala yake watoto wajikite zaidi katika kusoma kwa bidii ili wawe  viongozi bora na wenye maadili sahihi katika taifa letu.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya  siku ya mtoto wa Afrika ni: Maendeleo Endelevu 2030 " Imarisha Ulinzi na Fursa Sawa kwa Watoto."

Maadhimisho hayo ambayo kufanyika kila mwaka juni 16 yameadhimishwa kwenye mikoa mbalimbali nchini kote.