Ijumaa, 21 Julai 2017

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia ampongeza Mkuu wa Wilaya ya Korogwe kwa kusimamia vizuuri ujenzi wa miundombinu ya shule


Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhandisi Stella Manyanya amempongeza Mkuu wa Wilaya ya Korongwe Mhandisi Robert Gabriel kwa kuhamasisha wananchi kuchangia katika sekta ya elimu ambapo mchango huo wa wananchi umewezesha mradi wa ujenzi madarasa uliofadhiliwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia mradi wa Mradi wa lipa kulingana na matokeo kufanikiwa kwa kiwango kikubwa pamoja na ujenzi wa miundombinu mengine ya elimu inayofanywa na Halmashauri.

Mhandisi Manyanya ametoa pongezi hizo leo wilayani Korongwe Mkoani Tanga katika wakati wa ziara yake wilayani humo yenye lengo la kukagua utekelezaji wa ujenzi na ukarabati unaofanywa na Mradi wa Lipa kwa Matokeo (P4R). Amesema Mkuu wa wilaya huyo pamoja na kamati yake wameweza kuhamasisha wananchi kuchangia katika mradi huo na kuwezesha kujengwa madarasa zaidi ya yaliyokuwa yamelengwa hapo awali kwani wananchi walichangia nguvu kazi zao, mifuko ya saruji na vifaa vinine vya ujenzi.

Naibu Waziri ametolea mfano wa ujenzi wa miundombinu ya vyoo katika shule ya Msingi Kilimani ambapo wameweza kuijenga matundu ya vyoo 12 kwa gharama ya shilingi milioni 11 wakati sehemu nyingine ambazo ameshazitembelea wameshindwa kumaliza ujenzi wa vyoo kama hvyo kwa gharama hiyo.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Korongwe Mhandisi Robert Gabriel amemueleza Naibu Waziri kuwa Halmashauri yake imejipanga kuhakikisha wanaondoa tatizo la miundombinu ya madarasa katika wilaya yake kwa kujenga madarasa 360 pamoja na ofisi za walimu 70 ndani ya kipindi cha miezi 12 kwa kutumia nguvu za wananchi.

Katika ziara hiyo Mhe Naibu Waziri alitembelea shule za Msingi Kilimani, Bagamoyo, Matondoro, Kilole, Kwasemangube, Shule ya Sekondari Semkiwa pamoja na Chuo cha Ualimu Korogwe.











Hakuna maoni:

Chapisha Maoni