Ijumaa, 10 Novemba 2017

Kauli ya Serikali kuhusu udahili na utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu mwaka 2017/18 iliyotolewa na Prof.  Joyce Ndalichako (MB) - Bungeni, Dodoma; Novemba 09, 201

#Udahili wa wanafunzi walioomba kujiunga na vyuo vya elimu ya juu ulifanyika kwa awamu tatu na ulihusisha jumla ya vyuo na taasisi za elimu ya juu 67.
#Katika awamu ya kwanza majina 77,756 yakipokelewa TCU, wanafunzi 44,627 walichaguliwa.

#Baada ya uhakiki waombaji 36,831 waliidhinishwa na kujiunga na shahada ya kwanza. Waombaji 7,796 walikuwa na kasoro mbalimbali kwenye taarifa zao hivyo kukosa sifa ya kujiunga na vyuo.

#Awamu ya pili ililenga waombaji waliokosa udahili awamu ya kwanza ambapo jumla ya waombaji 19,488 walijitokeza na walioidhinishwa kuwa na sifa za kujiunga ni 9,525.
#Awamu ya tatu ilikuwa kwa ajili ya kutoa nafasi ya mwisho kwa wanafunzi waliokosa vyuo ambapo jumla ya waombaji 7,418 waliidhinishwa kujiunga na vyuo.

Hadi kukamilika kwa awamu ya  tatu waombaji 63,737  waliidhinishwa kujiunga na vyuo  na  waombaji 28,466 kati yao walikuwa wamechaguliwa zaidi ya chuo kimoja.

#Serikali katika mwaka wa fedha 2017/18 imepanga kutumia Shilingi Bilioni 427.54 kugharamia mikopo kwa ajili ya wanafunzi wenye uhitaji na waliodahiliwa na vyuo vya elimu juu hapa nchini.

#Mikopo hii ni kwa ajili ya wanafunzi 122,623 ambapo wanafunzi 30,000 ni wa mwaka wa kwanza na wanafunzi 92,623 ni wanaoendelea na masoma.

#Katika robo ya kwanza ya mwaka huu wa masomo, Wizara imepokea Shilingi Bilioni 147.06 kwa ajili ya ada za wanafunzi na kwa ajili ya kugharamia chakula, malazi, vitabu, viandikia na mahitaji maalum ya masomo.

#Utoaji wa mikopo umezingatia vigezo vilivyowekwa ambavyo ni ulemavu, uyatima na uhitaji hasa katika programu za kipaumbele.

*Changamoto Zilizojitokeza Katika Utoaji wa Mikopo. 
                           
#Baadhi ya waombaji kutozingatia mwongozo na maelekezo ya uombaji kwa kutoambatanisha nyaraka muhimu zinazothibisha uhitaji wao.

#Baadhi ya wanafunzi waliopangiwa mikopo kuamua kuripoti kwenye vyuo tofauti walivyothibitisha udahili wa awali ambapo mikopo yao  imelipwa kwenye vyuo tofauti na waliporipoti.

#Dhana ya mikopo ni ya elimu ya juu ni kwa ajili ya wanafunzi wote na hivyo hata wanafunzi wasio na sifa kulingana na vigezo kutaka wapate mikopo.

*Hatua Zilizochukuliwa Kukabiliana na Changamoto Zilizojitokeza. 

#Kupokea taarifa na nyaraka za ziada na kusahihisha taarifa za maombi kutoka kwa wahitaji walioshindwa kukamilisha taarifa husika wakati wa kipindi cha maombi.

#Kukamilisha utaratibu wa kufungua dirisha la rufaa ili baadhi ya wanafunzi watakaokuwa hawajapangiwa mikopi kufikia tarehe 10/11/2017 waweze kuwasilisha rufaa zao ili wale watakaofanikiwa kwenye rufaa wapangiwe mikopo kabla ya tarehe 30/11/2017.

#Kupokea taarifa za usajili za wanafunzi wenye mikopo ili wale ambao mikopo iko vyuo tofauti ihamishwe kwenye vyuo walivyoripoti.

#Serikali imeshawaagiza wakuu wote wa vyuo vya Elimu ya Juu kuacha urasimu katika utoaji wa fedha kwa wanufaika wa mikopo.

#Inasikitisha sana kuona kuwa baadhi ya vyuo vinadiriki hata kuwakataa wanafunzi waliowadahili wao wenyewe.

#Nampongeza Rais Dkt. Magufuli kwani haijawahi kutokea, fedha kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu zikatolewa mwezi mzima kabla ya vyuo kufunguliwa 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni