Jumatatu, 8 Januari 2018

Serikali kuimarisha Elimu Nje ya Mfumo Rasmi

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa. Joyce Ndalichako amesema Mkakati wa Serikali ni kuimarisha Elimu Nje ya Mfumo Rasmi ili kuwapa nafasi watoto wanaoshindwa kujiunga na Mfumo huo wa Elimu kuwa na fursa nyingine ya kupata Elimu na Ujuzi ambao utawasaidia katika kulileea Taifa Maendeleo .

Kauli hiyo ameitoa leo jijini Dar es salaam katika ofisi ndogo za Wizara alipokutana na kufanya mazungumzo na  balozi  wa Uingereza Sarah Cooke, balozi wa Sweden katrina Rangnitt na balozi wa Canada Alexandre leveque wanaowakilisha nchi zao hapa nchini
Waziri Ndalichako amewaambia Mabalozi hao kuwa Elimu Nje ya Mfumo usio Rasmi ipo kwa ajili ya kuwasaidia wale walioshindwa  kujiunga na Mfumo Rasmi wa Elimu, hivyo hata wale watakaopata ujauzito wanashauriwa kujiunga katika mfumo huo ili kuendelea na masomo yao mara baada ya kujifungua.

Profesa Ndalichako amesema lengo la serikali ni kuwapa fursa wanafunzi wanaokosa nafasi au wanaoacha shule kwa sababu mbalimbali waweze kupata Ujuzi na Elimu katika njia nyingine ikiwemo mafunzo ya ufundi katika Vyuo vya Ufundi Stadi na Vyuo vya Maendeleo ya Jamii mafunzo ambayo yatawawezesha kujiajiri ama kuajiriwa.

Akizungumzia Mkakati wa Serikali katika kupambana na changamoto za mtoto wa kike kupata elimu , Profesa Ndalichako alisema mpaka sasa serikali kupitia Programu ya lipa kulingana na Matokeo, EP4R imeshajenga zaidi ya mabweni 300 katika maeneo mbalimbali nchini hasa yale yaliyo katika mazingira magumu na kutoa wito kwa wafadhili mbalimbali kuunga mkono jitihada za Serikali kwa kuchangia ujenzi wa mabweni katika maeneo yenye mazingira magumu kwa  ili kuwasaidia wanafunzi wawezekufanya vizuri katika masomo yao.

Akizungumza kwa niaba ya Mabalozi wengine Balozi wa Sweden nchini Tanzania Katarina Rangnitt amesema wamefurahishwa sana kusikia kutoka kwa Waziri kuwa watoto wanaopata mimba shuleni wanapata fursa nyingine ya kupata Elimu na ujuzi nje ya mfumo usio rasmi ambao utawasaidia katika kuendeleza maisha na kuewa Elimu ndiyo nguzo pekee katika kujieletea Maendeleo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni