Alhamisi, 9 Agosti 2018

WAZIRI NDALICHAKO AIAGIZA NACTE KUFUNGIA VYUO VINAVYOTOA MAFUNZO KWA UBABAISHAJI


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako ameliagiza Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) kuendelea kufungia vyuo vinavyotoa  mafunzo kwa ubabaishaji  ili kulinda ubora wa Elimu na Ujuzi kwa wanafunzi.

Waziri Ndalichako ameyasema hayo Jijini Dar es salaam wakati akizindua Baraza la Uongozi la Taifa la Elimu ya Ufundi ambapo amewataka NACTE kufungia hata vyuo  vya serikali kama itabainika kutoa mafunzo yasiyo na ubora.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akimkabidhi Mwenyekiti mpya wa Baraza la Baraza la Uongozi la Taifa la Elimu ya Ufundi Prof. John Kondoro Sheria na Kanuni za Baraza hilo wakati wa uzindzi uliofanyika jijini Dar es Salaam

“Hatutaki kuwa na utitiri wa vyuo vingi ni bora kuwa na vichache lakini vitoe wahitimu wenye ujuzi na maarifa ambao wanaweza kuwa na mchango katika Taifa letu.” Amesisitiza Waziri Nalichako.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Leornald Akwilapo akizungumza na wananchi wa mtaa wa Majimatitu B Kata ya Kilungule mkutano huo ulifanyika katika viwanja vya shule mpya inayojengwa kwa ajili ya kupunguza mlundikano wa wanafunzi wa shule ya msingi Majimatitu A 

Pia Waziri Ndalichako amekagua Maendeleo ya ujenzi wa shule mpya ya Msingi inayojengwa Majimatitu Wilayani Temeke  yenye lengo la  kupunguza mlundikano wa wanafunzi katika shule ya Msingi Majimatitu A yenye wanafunzi zaidi ya 7000.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akikagua madaftari ya wanafunzi wa Darasa la pili katika shule ya Msingi ya Majimatitu A. Waziri Ndalichako alifika shuleni hapo kujionea mrundikano wa wanafunzi katika shule hiyo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni