Jumanne, 27 Februari 2018


INVITATION TO TENDER

UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

MINISTRY OF EDUCATION SCIENCE AND TECHNOLOGY



CONSTRUCTION WORKS FOR MPWAPWA TEACHERS COLLEGE

NATIONAL COMPETITIVE BIDDING (NCB)

SPECIFIC PROCUREMENT NOTICE (SPN):

Loan No. 2100150031995
Project ID No.: P-Z1-IB0-016
Tender No.:  ME-024/2017-18/HQ/W/14
1.         This Invitation for Bids follows the General Procurement Notice (GPN) for this project that appeared in UNDB online with reference number AfDB34-01/15 of 20th January 2015, and on the African Development Bank Group’s Internet Website.
2.         The United Republic of Tanzania has received Financing from the African Development Bank in various currencies towards the cost of Support to Technical Vocational Education and Training and Teachers Education (STVET-TE).  It is intended that part of the proceeds of this loan will be applied to eligible payments under the contract for Construction Works for MPWAPWA Teachers College.
3.         The Permanent Secretary, Ministry of Education, Science and Technology (MoEST) now invites sealed bids from eligible bidders who meet qualifications criteria as stated in Bidding Document and are registered with the Contractors Registration Board of Tanzania as Building Contractor in Class four and above for the construction works for MPWAPWA Teachers College
4.         Interested eligible bidders may obtain further information from and inspect the bidding documents at the office of Secretary, Ministerial Tender Board, Ministry of Education, Science and Technology, College of Business Studies and Law Universities of Dodoma (UDOM) Block 10, Room no.320, 40479 DODOMA, TANZANIA Tell: 026 – 2963533 from 08.00 to 15.00 hours, Mondays to Fridays inclusive, except on public holidays.

5.         A complete set of bidding documents may be purchased by interested bidders on the submission of a written application to the above address and upon payment of a non-refundable fee of TZS. 150,000.00(Tanzania shillings one hundred thousand only)
6.         The provisions in the Instructions to Bidders and in the General Conditions of Contract are the provisions of the African Development Bank Standard Bidding Document:  Procurement of Goods.
7.            Bids must be delivered to the above office on or before 10.30HRS on Tuesday, 27th Mach 2018 and must be accompanied by a bid security in acceptable form (in the form of bank guarantee) of Tanzanian Shillings Twenty Million (20,000,000/=).


8.            Bids will be opened in the presence of bidders’ representatives who choose to attend at 10.45HRS on Tuesday, 27th Mach, 2018 at the offices of Ministry of Education, Science and Technology, College of Business Studies and Law, Universities of Dodoma (UDOM) Block 10, Ground Floor, Conference Room.


Permanent Secretary
Ministry of Education, Science and Technology
UDOM Block 10, P.O. Box 10,
40479DODOMA


Jumatatu, 26 Februari 2018

China na Korea kuisaidia Tanzania katika Sekta ya Afya na Elimu.


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichoko ameishukuru Serikali ya Watu wa China kwa kukubali ombi  lililotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Magufuli la kufadhili  wataalam wa sekta ya Afya.

Waziri Ndalichako ametoa kauli hiyo hii leo alipotembelewa na Balozi wa China nchini Tanzania Wang Ke aliyefika katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kufanya mazungumzo kuhusu utaratibu wa kupata wanafunzi watakaofaidika na ufadhili huo.

Balozi Wang Ke amesema baada ya Rais wa China kupata maombi hayo ametoa ufadhili wa Serikali yake kwa wanafunzi 20 wa Kitanzania watakaopata ufadhili wa masomo katika Sekta ya Afya kutoka Serikali ya China kwa mwaka wa masomo wa 2018/2019 katika ngazi za Uzamili na Uzamivu.

Aidha, Balozi Wang Ke amesema mbali na ufadhili huo pia Serikali ya China itaendesha Mpango wa Mafunzo kwa wataalamu wengine 20 mpaka 30 wa Sekta ya Afya kwa muda wa mwezi mmoja nchini China, hivyo amemuomba Waziri  wa Elimu kusaidia katika kuratibu upatikanaji wa Wanafunzi na aina ya mafunzo ambayo yatasaidia katika kutatua changamoto katika Sekta ya Afya.

Katika hatua nyingine Waziri  Ndalichako amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya Korea Song Geum – Young  kwa lengo la kujadili ujio wa wabunge kutoka Bunge la Korea kwa ajili ya kutoa msaada katika Hospitali ya Tiba na Taaluma ya Mlongazila.

Waziri Ndalichako amemwambia balozi huyo kuwa Serikali bado inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kujenga mbiundombinu ya kuwezesha wanafunzi na wauguzi kuishi karibu na hospitali ya Taalum na Tiba ya Mlongazila. 

Waziri amesema kwa sasa serikali ipo katika ujenzi wa awamu ya kwanza ya Miundombinu itakayowezesha wanafunzi wapatao 1500 kuishi karibu na hospitali hiyo. 

Waziri Ndalichako amesema Hospitali hiyo imejengwa kwa lengo la kuongeza udahili wa wanafunzi mpaka kufikia wanafunzi zaidi ya 10,000 hivyo bado Miundombinu itakayowezesha kuchukua idadi hiyo ya wanafunzi pamoja na watumishi wa hospitali hiyo inahitajika.

Naye Balozi wa Jamhuri ya Korea amesema serikali yake bado itaendelea kusaidia katika uendeshaji wa hospitali hiyo pamoja na miradi mingine katika Sekta ya Elimu.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Korea  Song Geum – Young ofisini kwake ambapo kwa pamoja walijadiliana namna bora ya kuisaidia uboreshaji wa Miundombinu ya Hospitali ya Tiba na Taaluma ya Mloganzila.




 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa  Joyce Ndalichako akizungumza na Balozi wa China Wang Ke kuhusu ufadhili wa masomo katika Sekta ya Afya kutoka Serikali ya China kwa mwaka wa masomo wa 2018/2019 katika ngazi za Uzamili na Uzamivu. 






Alhamisi, 22 Februari 2018

Waziri wa Elimu ashiriki kuaga mwili wa Akwilina Akwiline.


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa  Joyce Ndalichako leo ameongoza Wananchi mbalimbali kuaga mwili wa aliyekuwa Mwanafunzi wa Chuo cha Usafirishaji (NIT) marehemu Akwilina Akwiline jijini Dar es salaam.
Akizungumza wakati wa kumuaga Marehemu Akwilina Waziri Ndalichako amesema msiba huo umemgusa kila Mtanzania kwa kuwa Marehemu amekutwa na umauti akiwa anatekeleza majukumu yake ya kielimu.

Aidha, Waziri Ndalichako amezitaka Mamlaka zinazohusika kuharakisha kufanya uchungizi ili wale wote watakaobainika kuhusuika na tukio hilo waweze kuchukuliwa hatua  kwa mujibu wa  sheria za nchi.

Viongozi wengine walioshiriki kuaga mwili wa Mwanafunzi huyo ni pamoja na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Hamad  Yussuf Massauni, Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi Atashasta Nditiye , Kamanda wa kanda Maalumu ya Dar e salaam Lazaro Mambosasa  na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Leonard Akwilapo.

Mwili wa Akwilina Akwiline tayari umesafairishwa kuelekea mkoani Kilimanjaro na mazishi yanatarajiwa kufanyika kesho mkoani humo.





Jumanne, 20 Februari 2018

Waziri Prof. Ndalichako aziagiza Taasisi za Elimu kufuata Taratibu, Kanuni na Sheria za nchi


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako amezitaka Taasisi zinazotoa Elimu ya Juu hapa nchini kufuata taratibu, Sheria na kanuni za nchi katika kuendesha Taasisi hizo.

Waziri Ndalichako ametoa kauli hiyo hii leo jijini Dar es Salaam alipofanya ziara ya kushtukiza katika Chuo Kikuu cha Kampla kilichopo Gongo la Mboto  ambapo amebaini kuwepo kwa idadi kubwa ya watumishi ambao hawana vibali vya Makazi  na Ajira.
Waziri Ndalichako amesema Chuo hicho kumekuwa na udanganyifu wa taarifa za kiutumishi ambapo watu walioajiriwa kama madereva na wahudumu wamekuwa wakiingizwa katika orodha ya watumishi  ambao ni Walimu huku wakijua watumishi hao hawana sifa za kuwa Walimu.

Waziri Ndalichako amesema baadhi ya walimu katika chuo hicho kutoka nje ya nchi wanakuja kama wanafunzi lakini wakifika Chuoni hapo wanahalalishwa na kuwa walimu ambao wanafundisha wanachuo bila kuwa sifa stahiki.

Profesa Ndalichako pia amekitaka chuo hicho kuhakikisha kinafuatilia kwa karibu nidhamu ya wanafunzi wanaosoma Chuo hapo kwa kuhakikisha wanazingatia na kufuata taratibu, kanuni na sheria za nchi.

“Nidhamu ni jambo la msingi sana, sasa hakikisheni wanafunzi wanaomaliza katika chuo hiki wanakuwa na nidhamu ikiwa ni pamoja na kuzingatia kanuni na taratibu za ndani  na nje ya nchi na siyo vinginevyo, maana kuna baadhi ya wanafunzi ambao nyaraka zinaonyesha wamemaliza kwenye Chuo hiki na wako nje ya nchi lakini hawana maadili, liangalieni hili kwa umakini,”alisema Profesa Ndalichako.

Kwa upande wake  Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dk. Anna Makakala  amezitaka Taasisi zote za Elimu nchini kuhakikisha zinatoa ushirikiano kwa ofisi hiyo ili kuepuka kukiuka taratibu na miongozo iliyowekwa na nchi.




Jumatatu, 19 Februari 2018

TAARIFA KWA UMMA



TAARIFA KWA UMMA
Nimepokea kwa masikitiko makubwa sana taarifa ya kifo cha Akwilina  Bafhata Akwiline aliyekuwa mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika Chuo cha Usafirishaji (NIT).
Kifo hicho kimetokea wakati askari wakiwa wanadhibiti maandamano yaliyokuwa yakifanyika tarehe 16/02/2018 kwenye eneo la Mkwajuni Wilaya ya kinondoni, jijijini Dar es salaam.

Napenda kutumia fursa hii kutoa pole sana kwa Familia ya Ndugu,  jamaa na marafiki wote wa Akwilini.  Pia napenda kutoa pole kwa Uongozi na Jumuia ya Chuo cha Usafirishaji, wanafunzi wote nchini na wananchi wote kwa ujumla.

Ndugu Akwilini ni binti aliyekuwa anatambua na kuthamini umuhimu wa Elimu, na alijitoa kuhakikisha kuwa anasoma kwa bidii kwa manufaa yake binafsi, familia yake na kwa manufaa mapana ya taifa taifa.  Kifo chake kimetokea wakati akiwa kwenye kutekeleza wajibu wake kama mwanafunzi wa kupeleka barua mahali alipokuwa anatarajia kufanya mazoezi kwa vitendo yatakayoanza tarehe 27/02/2018. Kifo hicho cha kusikitisha kimezima ndoto yake Serikali ikekipokea kwa masikitiko makubwa sana. 

Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Joseph Pombe Magufuli amesikitishwa  na kuhuzunishwa sana na kifo cha mwanafunzi Akwilini na anaungana na familia, ndugu jamaa na watanzania wote kuwapa pole za dhati kutokana na msiba huo. 
Serikali inatumia fedha nyingi kuwasomesha wanafunzi kuanzia Elimu msingi, sekondari na hutoa mikopo kwa wanafunzi wa Elimu ya juu kwa sababu tunatambua mchango wa Elimu katika maendeleo ya nchi yetu. Marehemu Akwilini alikuwa ni miongoni mwa wanufaika wa Mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu. 

Mimi  Waziri mwenye dhamana ya  sekta ya Elimu nimesikitika sana kuona binti huyo amepoteza maisha yake akiwa katika kutekeleza shughuli za kielimu.

Wizara yangu itagharamia shughuli zote za mazishi ya Marehemu Akwilina hadi hapo atakapopumzishwa katika makao yake ya milele. 
Namuagiza Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Dk. Leonard Akwilapo kusimamia shughuli zote za msiba huo hadi  Akwilina atakapozikwa katika nyumba yake ya milele. 

Nitumie fursa hii kuviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuwafikisha mara moja wahusika waliosababisha kutokea kwa tukio hilo kwenye vyombo vya sheria ili  wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria za nchi yetu.

Nawasihi sana watanzania wenzangu tujiepushe kukiuka tarataibu na miongozo inayokuwa inatolewa ikiwemo  maandamano na vitendo vyote ambavyo vinaweza kusababisha maafa kwa watu wasio na hatia.

Mungu aiweke roho ya Marehemu Akwilini mahala pema peponi Ameni

Imetolewa na:

Prof Joyce Lazaro Ndalichako
Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia.
18 / 02/2018


Katibu MKuu Akwilapo: awataka watumishi wa wizara yake kufanya kazi lea bidii na weledi


Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Leonard Akwilapo amewataka watumishi wa wizara hiyo kufanya kazi kwa bidii na  kuzingatia weledi katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku.

Dk. Akwilapo ameyasema hayo wakati wa kikao cha kwanza cha watumishi wa wizara hiyo kilichofanyika mkoani Dodoma tangu serikali itangaze rasmi kuhamishia makao makuu ya nchi mkoani humo.

Dk. Akwilapo amesema utii, ushirikiano,bidii na upendo mahali pa kazi miongoni mwa watumishi ndiyo silaha pekee ya kufikia malengo ambayo Wizara imejiwekea katika kuinua Sekta ya Elimu hapa nchini.

"Nipende kuwapongeza watumishi wote kwa kushiriki majukumu mbalimbali ya Wizara ikiwemo kuisimamia vyema miradi mbalimbali inayotekelezwa na Wizara, nawasihi sana tuusifanye kazi kwa kujitenga, ushirikiano miongoni mwetu ni jambo la msingi sana na tukiwa na Umoja basi mafanikio lazima yatapatika katika Sekta hii ya Elimu,"alisema Dk.Akwilapo.

Pia Katibu Mkuu Dk.Akwilapo amewataka watumishi kuwa na matumizi sahihi ya Teknolojia,kujibu barua mbalimbali kwa wakati pamoja na kushughulikia faili zinazofika kwenye ofisi zao ndani siku mbili  na siyo kuziacha zikae muda mrefu.


Kupitia kikao hicho watumishi pia walipata fursa ya kuwaaga viongozi ambao walitumikia Wizara hiyo ambao hivi sasa wamehamiahiwa Wizara nyingine na kuwakaribisha viongozi wapya ambao wamehamia kwenye Wizara hiyo.

Viongozi waliokaribishwa ni pamoja na Naibu Waziri William Ole  Nasha na Naibu Katibu Mkuu Profesa  James Mdoe na walioagwa ni Naibu Waziri Mhandisi Stella Manyanya na Profesa Saimon Msanjila ambaye hivi sasa ni Katibu Mkuu anayesimamia Sekta ya Madini.