Jumatano, 20 Agosti 2014

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI



TANGAZO KWA UMMA

MAPENDEKEZO YA MABORESHO YA MICHEPUO NA TAHASUSI ZA KIDATO CHA KWANZA MPAKA CHA NNE NA KIDATO CHA TANO NA SITA

Elimu ya sekondari katika ngazi ya Kidato cha Kwanza hadi cha Nne   imekuwa ikiongozwa na michepuo ya ama ya Sanaa, Sayansi, Ufundi na Biashara. Halika dhalika, masomo ya sekondari Kidato cha Tano na Sita yamekuwa ya kifundishwa kwa kutumia Tahasusi mbalimbali kulinga na mahitaji ya nchi ambazo kwa sasa ni PCM, PCB, PGM, CBG, EGM, CBA, CBG, CBN kwa Sayansi, na  HGL, HGK, HKL, KLF, ECA, HGE kwa Sanaa.

Mafanikio mbalimbali yamepatikana kwa kutumia mfumo huu tangu ulipoanza hadi sasa. Hata hivyo, kutokana na (a) nia ya nchi kupiga hatua zaidi katika maeneo mbalimbali ya maendeleo ya nchi kwa mujibu wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025, (b) mabadiliko ya mahitaji ya ulimwengu wa ajira na kazi na (c) kuendelea kukua kwa ugunduzi na ubunifu pamoja na matumizi ya Sayansi na Teknolojia katika maeneo mbalimbali, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imeona kuna umuhimu wa kupitia upya Michepuo na Tahasusi zilizopo ili ufundishaji uweze kwenda na wakati. Michepuo na Tahasusi hizo mpya zinatarajiwa kuanza kutumika katika mwaka wa masomo 2015/2016.

Ili kufanikisha maboresho hayo, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi inakaribisha wadau wote wa Elimu na Mafunzo kutoa mapendekezo ya jinsi gani Michepuo na Tahasusi za elimu ya sekondari ziundwe au kuanzishwa katika madarasa ya kidato cha Kwanza hadi Nne na Tano hadi Sita. Mwisho wa kutuma mapendekezo ni tarehe 31/10/2014. Wadau wote mnahamasishwa kutoa maoni yenu kupitia njia mbalimbali ikiwemo vikao ama kwa kuwasiliana moja kwa moja na wizara. Majumuisho ya mapendekezo ya tawekwa kwenye magazeti na tovuti kwa maoni na hatua za mwisho katika kukamilisha maboresho haya.

Mapendekezo ya Michepuo naTahasusi mpya yatumwe kwa anuani ifuatayo:

Katibu Mkuu,
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi,
7 Mtaa wa Magogoni,
11479 DAR ES SALAAM.




Elimu Bora Inawezekana; Timiza Wajibu Wako


KATIBU MKUU

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUN DI

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni