Ijumaa, 28 Oktoba 2016

Balozi wa Canada amtembelea Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia ofisini kwake


Balozi wa Canada Ian Myles  akisisitiza jambo kwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Joyce Ndalichako  wakati Balozi huyo alipofika ofisini kwake kumsalimia. Katika kikao hicho Balozi wa Canada aliahidi serikali yake kuendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania katika kuboresha elimu


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako akisisitiza jambo kwa balozi wa Canada Ian Myles aliyefika ofisini kwake kujitambulisha ambapo pamoja na mambo mengine walizungumzia Mradi wa kuboresha Elimu ya Ualimu.


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako akizungumza na Balozi wa Canada Ian Myles pamoja na Susazn Steffen Kansela Mkuu Ushirikiano na Maendeleo kutoka ubalozi wa Canada waliofika ofisini kwake kujitambulisha ambapo pamoja na mambo mengine walizungumzia ushirlikiano kati ya serikali hizi mbili katika kuboresha elimu.


Wakurugenzi kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Gerald Mweli Kaimu Mkurugenzia wa Mipango na Sera (Mwenye shati Jeupe), Aletaulwa Ngatara Mkurugenzi Msaidizi Sera wa kwanza kulia na Mbarak Said  Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje  na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifiatilia kwa makini mjadiliano kati ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia na Balozi wa Canada.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni