Ijumaa, 21 Oktoba 2016

Rais Dkt. John Pombe Magufuli aweka Jiwe la Msingi la ujenzi wa mabweni ya Chuo Kikuu UDSM


  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na Jumuiya ya wanachuo wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Watumishi wa Serikali na wananchi kabla ya kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Mabweni ya Chuo Kikuu cha UDSM.


      Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akiongea na Jumuiya ya wanachuo wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Watumishi wa Serikali na wananchi waliofika kushuhudia uwekeaji wa jiwe la msingi wa ujenzi wa mabweni ya chuo hicho.


   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe wakati wa uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa mabweni ya Chuo Kikuu cha UDSM wengine katika picha ni Mama Janeth Magufuri, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Maimuna Tarishi na Naibu Katibu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leornad Akwilapo


    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa mabweni ya Chuo Kikuu cha UDSM uliofanyika leo katika viwanja vya chuo hicho.


    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Mama Janeth Magufuri, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia , Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Maimuna Tarishi na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam Prof. Rwekaza Mkandara wakisikiliza kwa makini taarifa za ujenzi wa hosteli hizo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu Wakala wa Majengo Tanzania Elius Mwakibinga (hayupo pichani)


      Baadhi ya wafanyakazi wanao husika na ujenzi wa hosteli za Chuo Kikuu cha UDSM wakimsiliza Rais Dkt. John Pombe Magufuri (hayupo pichani)alipokuwa akiongea katika uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa mabweni ya Chuo Kikuu cha UDSM uliofanyika leo katika viwanja vya chuo hicho

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni