Ijumaa, 4 Novemba 2016

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia yakabidhiwa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii


Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Sihaba Mkinga akimkabidhi  Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Maimuna Tarish  baadhi ya nyaraka mbalimbali zinazohusu Vyuo vya Maendeleo ya Jamii ambavyo sasa vitakuwa vikiendeshwa na kusimamiwa  na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na anayeshuhudia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Saimon Msanjila.


Katibu Mkuu Wizara za Elimu, Sayansi na Teknolojia Maimuna Tarish akizungumza na watendaji wa Wizara za Elimu, Sayansi na Teknolojia na Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  wakati wa  makabidhiano ya Vyuo vya Maendeleo ya Jamii yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa wizara.



Makatibu wakuu wa Wizara za Elimu, Sayansi na Teknolojia Maimuna Tarish na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  wakiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa wizara hizo  mara baada ya makabidhiano ya Vyuo vya Maendeleo ya Jamii.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni