Jumatano, 18 Oktoba 2017

Waziri Ndalichako azindua ufadhili wa wanafunzi unaotolewa na Barclays


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako amewataka wanafunzi kutumia mitandao ya kijamii kwa ajili ya kupata taarifa zitakazowasaidia kutekeleza fursa mbalimbali za kujiletea Maendeleo.
Waziri Ndalichako ameyasema hayo leo  wakati wa uzinduzi wa Twende kazi na Balozi mwanafunzi unaohusu ufadhili wa masomo kwa wanafunzi  23 wa shahada ya kwanza ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam na kusisitiza kuwa taasisi nyingine ziige mfano huo wa Barclays wa kufadhili wanafunzi.

Pia Barclays imewasaidia vijana 32 Kati ya 200 kuwatafutia ofisi ili kufanya kazi kwa vitendo kwa ajili ya kuwajengea uwezo wa kuwa tayari kwa kazi.

Uzinduzi huo pia umehudhuriwa na Mkurugenzi wa Elimu ya Juu, Profesa Sylivia Temu.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni