Jumatatu, 22 Januari 2018

Wizara ya Elimu yatoa msimamo kuhusu Shule kufukuza Wanafunzi kwa kutofikia wastani.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia  Profesa Joyce Ndalichako amekutana na kufanya mazungumzo na baadhi ya Viongozi wa wamiliki wa shule binafsi za sekondari ambapo kwa pamoja  wamejadili utekelezaji Wa waraka Namba. 7 unaokataza wanafunzi kufukuzwa shule kwa sababu ya kutofikisha wastani wa ufaulu uliowekwa na shule.

 Waziri Ndalichako ameeleza ameeleza kuwa chimbuko la waraka huo ni baadhi ya shule kufukuza idadi kubwa ya wanafunzi wakiwa Mwaka wa mwisho wa masomo yao kwa kigezo cha kutotimiza wastani unaotakiwa kitendo ambacho amekielezea kuwa kuwa ni cha kibaguzi na ki-unyanyasaji. 

" Mfano  shule ya sekondari Pandahil ambayo imefukuza watoto 148, shule ya sekondari star high imefukuza wanafunzi 49 hizo ni baadhi tu, Aidha, ameeleza kuwa   Wakati Bunge na Serikali ikisikitika pale Wasichana wanapopata uja uzito na kuacha shule, Waja sekondari na Musindi sekondari zimefukuza wanafunzi wa kike 15 kila moja kwa kigezo cha ufaulu mdogo.

Waziri huyo amesisitiza kuwa wizara itaendelea kusimamia utekelezaji wa waraka huo na amewataka Viongozi hao kuweka utaratibu mzuri kwa wanafunzi walio na uwezo mdogo badala ya utaratibu uliopo sasa wa kuwafukuza shule na hivyo kuwaacha wakiwa hawana pa kwenda.

Kwa upande wao viongozi wa wamiliki wa shule wameeleza kuwa utekelezaji wa waraka huo utasababisha kushukuka kwa Ubora Wa ufaulu katika shule zinazomilikiwa na watu binafsi.


Kikao hicho pia kilihudhuriwa  na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt Leonard Akwilapo kikao ambacho kimefanyika jijini Dar es salaam.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni