Jumatatu, 2 Julai 2018

WAZIRI NDALICHAKO AMEWATAKA WATAFITI KUTAFSIRI MATOKEO YA TAFITI KUWA BIDHAA NA HUDUMA


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amewataka watafiti wa afya nchini kupanga mipango ya utafiti kuzingatia matakwa ya wateja wanaowahudunia na kutafsiri matokeo ya tafiti hizo kuwa bidhaa na huduma.

Waziri Ndalichako ametoa kauli hiyo wakati wa kongamano la sita la kisayansi jijini Dar es Salaam na kusisitiza  kuwa utafiti unapotafsiriwa unaweza kubadilisha na kuboresha huduma zinavyotolewa pamoja na kusaidia taifa kufikia uchumi wa viwanda.  


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolijia Pfro . Joyce Ndalichako akizungumza wajumbe (hawapo Pichani) wa kongoamano la sita la Kisayansi lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) ambapo aliwasisitiza kupanga mipango ya utafiti kuzingatia matakwa ya wateja wanaowahudunia na kutafsiri matokeo ya tafiti hizo kuwa bidhaa na huduma

Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Prof. Andrea Pembe amesema tafiti zitakazowasiliwashwa ni pamoja na masuala ya Afya ya Uzazi, Magonjwa yasiyo ya kuambukizwa, na magonjwa yanayoambukiza, Sera ya Afya, Madawa ya jadi na mbadala na Sayansi ya madawa.

Kauli mbiu ya Kongamano hilo ni “Uimarishaji wa Uchumi wa Viwanda kupitia Tafiti za Afya kwenye nchi zenye kipato cha chini”.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolijia Pfro . Joyce Ndalichako akipata maelezo kuhusu dawa mbalimbali za usafi zilizotengenezwa na wadau wa afya wakati wa  kongoamano la sita la Kisayansi lililofanyika Jijini Dar es Salaam

Lengo la Kauli Mbiu hiyo ni kusisitiza umuhimu wa matumizi ya matokeo ya tafiti za Kisayansi za afya katika kuchangia uimarishaji wa uchumi wa viwanda.
Kongamano hilo la kisayansi limeandaliwa na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) na limeshirikisha jumla ya washiriki na wajumbe zaidi ya 400 kutoka nchini na nchi za Rwanda, Uingreza, Japan, Uturuki, Italy, Marekani na wenyeji Tanzania.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolijia Pfro . Joyce Ndalichako akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa kongoamano la sita la Kisayansi lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni