Jumapili, 19 Agosti 2018

SERIKALI KUTUMIA MBINU ZOTE ZA UFUNDISHAJI KUWEZESHA WATOTO KUJIFUNZA


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Joyce Ndalichako amesema Serikali itatumia mbinu zote za ufundishaji ili kuwezesha watoto kujifunza kwa ufanisi.

Waziri Ndalichako amesema hayo jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa ufundishaji wa maudhui yaliyoandaliwa kwa mfumo wa kietroniki ambayo yatatumia Vikaragosi (Cartoon) kufundishia watoto wa madarasa ya chini.

 Waziri Ndalichako amesema njia hii Itasaidia watoto kuelewa kwa  urahisi kwani wapo  watoto wanaoelewa kwa kuona, kushika na kisikiliza.




Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akizungumza na Wadau wa Elimu ( Hawapo Pichani)  wakati wa uzinduzi wa ufundishaji wa maudhui yaliyoandaliwa kwa mfumo wa kietroniki ambayo yatatumia Vikaragosi (Cartoon)


"ikumbukwe kwamba hakuna njia bora kuliko nyingine katika kufundisha, wapo watoto  wanaoelewa zaidi kwa kuona, kusilikiza ama Kufanya kwa vitendo hivyo ni muhimu kutumia njia zote ili tusiache mtoto yeyote bila kuelewa" Amesisitiza Waziri Ndalichako

Waziri Ndalichako amesema matumizi ya Vikaragosi yataleta ari kwa watoto kujifunza kwani wakati wa majaribio ya vikaragosi hivyo walionyesha hali ya kutaka kujifunza kwa kutumia.


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akionyesha DVD zenye maudhui ya Kietroniki ambazo zitatumika kufandishia madarasa ya chini wakati wa uzinduzi wa ufundishaji wa maudhui yaliyoandaliwa kwa mfumo wa kietroniki ambayo yatatumia Vikaragosi (Cartoon)

Aidha, Waziri wa Elimu amewataka Maafisa Elimu Kata kote nchini kuhakikisha wanafatilia kwa ukaribu ufundishaji kwa kutumia Vikaragosi hivyo pindi  vitakaposambazwa shuleni.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni