Jumatatu, 27 Agosti 2018

WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUANDIKA HABARI ZA SAYANSI NA TEKNOLOJIA

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia DK Leonard Akwilapo amewataka Waandishi wa habari nchini kujikita katika kuandika habari za Sayansi, Teknolojia na Ubunifu ili kuleta matokeo chanya katika kuelekea uchumi wa viwanda. 

Akizungumza wakati wa kutoa tuzo za umahiri kwa waandishi wa habari wa masuala ya Sayansi na Teknolojia zilizoandaliwa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia kupitia Jukwaa la Bioteknolojia kwa Kilimo jijini Dar es Salaam amesema kuwa Dunia inategemea Sayansi na Teknolojia katika kuleta mabadiliko  endelevu ya kimaendeleo
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Leonard Akwilapo  akimkabidhi mmoja wa washindi wa tuzo za umahiri kwa waandishi wa habari ya Sayansi na Teknolojia zilizoandaliwa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia kupitia Jukwaa la Bioteknolojia kwa Kilimo zilizofanyika jijini Dar es Salaam

Aidha, ameipongeza tume hiyo kwa kuona umuhimu wa kutoa taarifa ya nini inafanya kwa wananchi kwa kuwahusisha waandishi wa habari ambao wamekuwa wakitoa taarifa hizo kwa jamii kupitia vyombo vya habari

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia Dk. Amos Nungu amesema tuzo hizo zimeshirikisha kazi 56 kutoka katika vyombo 10 vya habari na kutoa wito kwa Waandishi wa Habari kujitokeza kwa wingi kushiriki katika kuelimisha jamii mambo mbalimbali yanayohusu Sayansi na Teknolojia.

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Leonard Akwilapo  akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wanasayansi (hawapo pichani) wakati wa kutoa tuzo za umahiri kwa waandishi wa habari wa Sayansi na Teknolojia ambapo amewataka waandishi wa habari kujikita katika kuandika masuala ya sayansi na teknolojia ili kuwezesha wananchi kufikia uchumi wa viwanda wakiwa na taarifa sahihi

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni