Jumamosi, 10 Novemba 2018

WAZIRI NDALICHAKO AVITAKA VYUO KUFUATA MIONGOZO KATIKA KUTOA ELIMU



Serikali imevitaka vyuo vyote vya Elimu ya Juu nchini kuzingatia kanuni na miongozo  inayotolewa na Baraza la Taifa la Ufundi (NACTE) na Tume ya vyuo  Vikuu Nchini (TCU) katika kutoa elimu ili kuepuka  kufungiwa au kufutiwa udahili.

Kauli hiyo ya serikali   imetolewa na Waziri wa Elimu, Sayansi naTeknolojia Prof. Joyce Ndalichako katika mahafali ya 53 ya Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kampasi ya Dar es Salaam, ambapo amesema serikali kupitia TCU na NACTE itaendelea kusimamia ubora wa Elimu na kuvifungia vyuo vyote vinavyotoa elimu chini ya kiwango.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akiwa katika maandamano ya kitaaluma wakati wa mahafali ya chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kampasi ya Dar es Salaam.

Waziri Ndalichako amesema kuna baadhi ya Vyuo ambavyo vimekuwa havifuati taratibu na miongozo inayotolewa na TCU na NACTE na kusababisha usumbufu kwa wanafunzi pale vinapotakiwa kufungiwa, na kusisitiza kuwa hatua zinazochukuliwa na Taasisi hizo  ni endelevu na kuwa lengo ni kuhakikisha wahitimu wanapata Elimu bora itakayowawezesha kujiajiri ama kuajiriwa.

 Waziri Ndalichako pia amewataka Wahadhiri wenye tabia yakuficha matokeo ya wanafunzi kwa madai ya kukosa maslahi yao kutoka kwa mwajiri  kuacha mara moja tabia hiyo kwani imekuwa ikiwasumbua wanafunzi ambao hawana hatia.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akizungumza na wahitimu katika mahafali ya Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kampasi ya Dar es Salaam amewataka kuwa wanafunzi kuwa mabalozi wazuri na wazalendo katika kazi zao baada  ya kuajiriwa ama kujiajiri.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo Cha CBE Prof. Emanuel Mjema amesema chuo hicho kinakabiliwa na changamoto ya uvhakavu wa miundombinu kutokana na Chuo hicho kuwa  cha muda mrefu,  hivyo Marion a serikali kukipatia udhamini ili kiweze kukopa katika Taasisi za fedha ili kuboresha miundombinu hiyo.




Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akimbalisha  mmoja wahitimu wa Shahada ya Uzamili ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano kwa Maendeleo katika mahafali ya Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kampasi ya Dar es Salaam.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni