Jumatano, 30 Januari 2019

WAZIRI NDALICHAKO AITAKA TAKUKURU KUCHUNGUZA MRADI WA UJENZI VETA YA MKOA GEITA.


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako ameitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuchunguza mchakato wa upatikanaji wa zabuni ya ujenzi wa Mradi wa Chuo Cha Ufundi stadi VETA mkoani Geita unaotekelezwa na Kampuni ya ukandarasi inayojulikama kama SkyWard.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akikagua mradi wa ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi, VETA mkoani Geita wakati wa ziara yake ya mkoani humo.

Waziri huyo amesema hajaridhishwa na ujenzi wa mradi huo na kuwa hadi sasa tayari ni miezi mitano  na kwa mujibu wa mkataba bado miezi sita mradi ukabidhiwe, lakini inavyoonekana ni kuwa kampuni hiyo tayari ilishaonesha kushindwa kazi ambayo walishapewa ya ujenzi wa Chuo Cha Ualimu Ndala.

“Mkandarasi hii Serikali siyo ya kuichezea, mwaka mzima sasa bado mko asilimia ambazo haziridhishi pia hakuna kasi ya majengo na hakuna vibarua wanaoendelea na kazi, mnadeni Chuo cha ualimu Ndala, na hapa tena  kwenye ujenzi wa Chuo cha VETA Geita kuna tatizo na hata mazingira ya kumpa huyu mkandarasi kazi, niwaonye watu wa Idara ya manunuzi pale Wizarani kuacha kutoa kazi kwa watu wasiokuwa na uwezo,” anasema Waziri Ndalichako,
Muonekano wa moja ya jengo katika mradi wa ujezni wa chuo cha Ufundi Stadi Mkoani Geita, ambapo Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amemtaka mkandarasi kukamilisha ujenzi huo katika muda uliopangwa na si vinginevyo.

Waziri huyo yuko mkoani Geita kwa ziara ya kikazi ya kukagua miradi ya ujenzi wa vyuo vya Ufundi stadi vya Geita na Chato.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akiwa ameambatana na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Geita wakati wa ziara ya kukagua mradi wa ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi kinachojengwa mkoani humo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni