Jumatano, 30 Januari 2019

WAZIRI NDALICHAKO ASEMA CHUO CHA UFUNDI STADI MKOANI KAGERA KUANZA KUJENGWA


Serikali imekamilisha miundombinu yote muhimu ikiwemo Maji, umeme na barabara kwa ajili ya kuanza kwa ujenzi wa Chuo cha Ufundi stadi VETA mkoani Kagera.

Kauli hiyo ya Serikali imetolewa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako baada ya kuzindua chanzo cha Maji ambacho kitatumika kwa ajili ya kujenga VETA hiyo katika kijiji cha Burugo, Kwenye halmashauri ya Bukoba.

“Dhamira ya Serikali ya awamu ya Tano ni kuwa nchi ya uchumi wa kati hadi ifikapo mwaka 2025 ili kutimiza malengo hayo ndiyo serikali imewekeza zaidi katika kujenga vyuo vya Ufundi stadi ili kuwa na wataalamu wa kati na wa kutosha watakaotumika kwenye viwanda hapa nchini,” alisisitiza Waziri Ndalichako.


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akizindua chanzo cha maji kitakachotumika kujenga chuo cha Ufundi stadi, VETA mkoani Kagera na kuwa ujenzi huo unatarajiwa kuanza muda wowote baada ya serikali kukamilisha miundombinu inaayohitajika kama vile maji, umeme na barabarana.

Awali akipokea taarifa ya mkoa huo kuhusu sekta ya Elimu, Waziri Ndalichako ameonesha kutoridhishwa na hatua za ujenzi wa matundu ya vyoo katika shule za msingi mkoani humo na kuzitaka mamlaka husika kutafuta ufumbuzi ili kuweka mazingira rafiki kwa wanafunzi.

Waziri Ndalichako pia ametembelea na kukagua ujenzi unaoendelea wa Chuo cha Ufundi Stadi Karagwe ambapo amemtaka Mkandarasi kuhakikisha kazi hiyo inakamilika katika muda uliopangwa.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akikagua mradi wa ujenzi wa chuo cha Ufundi stadi VETA, (KDVTC) Wilayani Karagwe mkoani Kagera ambapo waziri amemuelekeza mkandarasi kukamilisha ujenzi katika muda uliopangwa.


Waziri Ndalichako pia alitembelea Shule ya Bukoba Sekondari ambayo paa za shule hiyo ziliezuliwa kufuatia mvua kubwa Iliyoambatana na upepo na hivyo kulazimika wnafunzi wa shule hiyo kuhamishiwa katika shule ya sekondari Ihungo na wengine katika shule ya Sekondari Omumwani.

Wakala wa majengo ambaye ndiyo Mkandarasi wa mradi wa ujenzi wa Chuo cha Ufundi Karagwe,  Kilichopo Wilayani Karagwe akijadiliana Jambo na Waziri Ndalichako wakati Waziri akikagua ujenzi wa chuo hicho.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni