Jumatatu, 4 Februari 2019

DKT. AKWILAPO AMEWATAKA WATUMISHI KUFANYA KAZI KWA KUZNGATIA KANUNI, TARATIBU NA SHERIA ZA KAZI


Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo amewataka watumishi kufanya kazi kwa kuzingatia kanuni, taratibu na sheria za kazi pamoja na kujiepusha na vitendo vya rushwa.

Dkt. Akwilapo ameyasema hayo Jijini Dodoma wakati wa mkutano wa pamoja na watumishi wa Wizara hiyo wenye lengo la kupitia utendaji kazi wa wizara kwa mwaka 2018 na kuweka malengo ya utekelezaji wa majukumu kwa mwaka 2019.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo akizungumza na Watumishi wa Wizara hiyo (hawapo pichani), wakati akifungua mkutano wa pamoja uliofanyika Jijini Dodoma leo, ambao amewataka watumishi kufuata kanuni, taratibu na sheria za kazi pamoja na kujiepusha na vitendo vya rushwa katika utekelezaji wa majukumu yao. 


Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia  kutoka  Idara na Vitengo wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu Dkt. Leonard Akwilapo wakati wa mkutano wa pamoja wa Watumishi wa Wizara hiyo, mkutano huo umefanyika jijini Dodoma.

Katibu Mkuu huyo pia amewataka watendaji wa Wizara hiyo kuendelea kuwahudumia wateja kwa lugha nzuri na kuhakikisha huduma zinatolewa katika muda muafaka kwa lengo la kuepusha malalamiko.

“Nichukue fursa hii kupitia mkutano wa wafanyakazi wote kuwataka kutekeleza majukumu yenu kwa kufuata taratibu na sheria za kazi pamoja na kujiepusha na vitendo vya rushwa ili nchi iweze kufikia malengo ambayo imejiwekea. Kila mmoja atomize wajibu wake katika eneo lake naamini kwa kufanya hivyo tutafanikiwa,” alisisitiza Dkt. Akwilapo.

Watumishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (Makao Makuu) wakiwa katika Mkutano wa pamoja ambapo Katibu Mkuu ameelekeza watumishi kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa wateja na zitolewe katika muda muafaka.

Mkutano   wa pamoja wa Wafanyakazi wa Wizara hiyo hufanyika kila mwaka kwa lengo la kujitathmini katika utekelezaji wa majukumu ambayo Wizara inakuwa imejiwekea.

Mkutano wa pamoja wa Viongozi na watumishi wa Wizara wenye lengo la kupitia utendaji kazi wa Wizara kwa mwaka 2018 na kuweka malengo ya utekelezaji kwa mwaka 2019.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni