Ijumaa, 19 Aprili 2019

NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA ELIMU AKAGUA MRADI WA UJENZI MABWENI YA WANAFUNZI MZUMBE


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe ametembelea Kampasi Kuu ya Chuo Kikuu Mzumbe na kukagua mradi wa ujenzi wa mabweni ya wanafunzi unaoendelea katika eneo la Maekani

Akizungumza mara baada ya kukugua mradi huo mjini Morogoro, Prof. Mdoe amemuagiza mkandarasi “National Service Corporation Sole” (SUMA JKT) kukamilisha 
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe akikagua mradi wa ujenzi wa wa mabweni ya wanafunzi unaoendelea katika eneo la Maekani mkoani Morogoro.

"Serikali haitavumilia kucheleweshwa kwa mradi huu ambao ni muhimu kwa chuo katika kuondoa tatizo la malazi kwa wanafunzi"amesisitiza Prof. Mdoe

 Prof. Modoe  amewaagiza SUMA JKT  kuongeza vibarua na wafanyakazi kwa ajili ya kufanya kazi hiyo kwenda kwa haraka zaidi ili ukabidhiwe kwa wakati, hivyo kawashauri kuwa na zamu ili kukamilisha mradi huo.

Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. Ganka Nyamsogoro  amesema mabweni hayo ya wanafunzi yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi zaidi ya 1000 katika eneo la Maekani, Kampasi Kuu. umefadhiliwa na serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe akiongea na viongozi wa Chuo Kikuu Mzumbe mara baada ya kukagua mradi wa ujenzi wa wa mabweni ya wanafunzi unaoendelea katika eneo la Maekani mkoani Morogoro.

Nyamsogoro amesema mradi huo unatarajiwa kukamilika tarehe 19 April 2019 na gharama yake ni kiasi cha shilingi  billioni 6.5 fedha ambazo zimetolewa na serikali kupitia  Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Kwa upande wake msimamizi wa  mradi huo kutoka Suma jkt Eng. Focus Odecho wamemhakikishia Naibu Katibu Mkuu huyo kuwa ujenzi wa mabweni hayo  utakamilika ndani ya muda uliopangwa.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni