Ijumaa, 2 Agosti 2019

MAONESHO YA WANASAYANSI WATAFITI WACHANGA

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako  amesema Serikali inatambua umuhimu wa Sayansi Teknolojia na Ubunifu ktk maendeleo ya taifa letu na hivyo itaendelea kusimamia na kuendeleza wanasayansi wabunifu  nchini.
Amesema hayo wakati wa ufunguzi wa maonesho ya tisa ya wanasayansi watafiti wachanga nchini yanayoandaliwa na taasisi ya Young Scientists Tanzania, (YST) jijini Dar Es Salaam
Maonesho hayo huwahusisha wanasayansi wanafunzi kutoka shule za sekondari kote nchini , kuonesha tafiti walizofanya kupitia mpango wa YST. 
Ndalichako amewapongeza wanafunzi walioshiriki kwa kuonesha tafiti zilizofanywa kisayansi na ubora na pia kwa kutumia teknolojia katika kubuni mambo mbalimbali  na mifumo inayotoa utatuzi wa  changamoto za jamii yetu. 
Amepongeza walimu wanaoshiriki katika mpango huo kwa kuweza kutoa hamasa kwa wanafunzi kupenda masomo ya sayansi na hisabati na kwa kufundisha vizuri hali ambayo inajionesha kupitia kazi bora za wanafunzi wao.


  










Hakuna maoni:

Chapisha Maoni