Alhamisi, 6 Aprili 2017

DKT AKWILAPO KATIBU MKUU MPYA WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli leo amemuapisha Dkt Leonard Akwilapo kuwa Katibu Mkuu Mpya wa Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia baada ya aliyekuwepo Maimuna Tarishi kuhamishiwa ofisi ya Waziri Mkuu. Kufuatia uteuzi huo nafasi yake aliyokuwa akiishika katika Wizara hiyo kama Naibu Katibu Mkuu  imechukuliwa na Dkt Ave Maria Semakafu ambaye alikuwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Afya  na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS)

Akizungumza na wafanyakazi wa Wizara hiyo mara baada ya kuapishwa Dkt Akwilapo amewataka wafanyakazi  kufanya  kazi  kwa bidii na weledi mkubwa ili kufikisha malengo ambayo tumejiwekea ikiwa ni pamoja na kutatua changamoto za watanzania walio  wengi. Alisema Wizara ya Elimu ni Kubwa, nzito na ina mambo mengi pamoja na changamoto zake tutumie mbinu  tulizo nazo kuhakikisha tunatatua changamoto hizo bila matatizo.

 “ katika kutatua changamoto mara nyingi hapakosi kuleta kusigana hivyo tuvumiliane tufanye kazi kwa pamoja ili tuweze kutimiza malengo makubwa ya Wizara” alisisitiza Dkt Akwilapo

Dkt Akwilapo amesema anaamini katika Wizara ya Elimu ana azina ya kutosha kwa kuwa amekulia katika Wizara hiyo hivyo anaifahamu vizuri na anaamini uzoefu alionao utasaidia kutatua changamoto zilizopo.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt Ave Maria Semakafua amesema wafanyakazi wote tuwe na lengo moja la kusonga mbele katika kufanya kazi  na kutatua changamoto kwa pamoja kwani wizara ya Elimu  ni kubwa na changamoto zake  ni kubwa pia.  Amesema changamoto hizo zinaanzia katika makuzi na malezi, ili kuhakikisha watoto wote wenye umri wa kwenda shule wanaandikishwa sisi kama walezi  tuhakikishe tunafuatilia kwa ukaribu. Amesema yeye ni mwanaharakati amekuwa akipigania haki za watoto wa kike kuhakiksha wanapata elimu lakini sasa suala la elimu kwa watoto wote linatakiwa  kupiganiwa kwani wapo watoto wa kiume wanaopata changamoto zinazo haribu maisha yao na kukatiza masomo yao.


Akizungumza kwa niaba ya wafanyakazi Bwana Nicholaus Moshi kiongozi wa Chama cha Walimu tawi la Wizara ya Elimu amesema tunawapongeza kwa nafasi walioshika kwani wameteuliwa kati ya watanzania wengi kuweza kuongoza Wizara hiyo na kwamba  tunaahidi kufanya kazi kwa bidii ili tuweze kutimiza malengo ya watanzania walio wengi kwenye elimu ya watoto wao.













Jumatatu, 27 Machi 2017

KATIBU MKUU AKAGUA UJENZI WA CHUO CHA VETA, MKOANI MOROGORO.

Katibu mkuu wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia  Maimuna Tarishi ametembelea na kukagua ujenzi unaoendelea wa majengo ya chuo cha Veta kilichopo kihonda  mkoani Morogoro.
Katibu Mkuu Tarishi amekagua  jengo la utawala na majengo mawili ya karakana ikiwemo karakana ya umeme wa magari na karakana ya  ufundi seremala, na kuwa ujenzi wa majengo hayo  kwa hivi sasa uko katika hatua za kupauliwa.







Ijumaa, 24 Machi 2017

NAIBU KATIBU MKUU AFUNGA KONGAMANO LA WADAU WA ELIMU

Naibu Katibu Mkuu  wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt Leonard akifunga kongamano la siku tatu la wadau wa Elimu waliokutana kuzungumzia masuala ya uongozi na usimamizi wa masuala ya Elimu katika karne ya 21 lililofanyika katika Chuo Kikuu cha Aga Khan, Taasisi ya kuendeleza Elimu Afrika Mashariki.



UZINDUZI WA MAKTABA.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt Leonard Akwilapo akizindua maktaba ya Makumbusho ya Taifa Baada ya kupokea vifaa vya maktaba hiyo ikiwa pamoja na vishikwambi (TABLETS  kutoka kwa  Serikali ya  Watu wa Korea kupitia mradi wa THANK YOU SMALL LIBRARY.





Jumatano, 22 Machi 2017

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAENDELEO NA HUDUMA ZA JAMII IKIKAGUA JENGO LA TEACHING TOWER LILILOPO DIT.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhandisi Stella Manyanya akiwa na baadhi ya wajumbe wa kamati ya Bunge ya Maendeleo na huduma za jamii wakikagua jengo la kufundishia, ambalo ndani yake kuna ofisi, chumba cha ujasiriamali, na vyumba vya madarasa, (Teaching Tower)








Jumanne, 21 Machi 2017

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAENDELEO NA HUDUMA ZA JAMII YATEMBELEA MLOGANZILA.

Kamati ya bunge ikiongozwa na Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya bunge ya Maendeleo na huduma za jamii, Peter Serukamba na baadhi ya viongozi wa Wizara akiwemo Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako, Naibu waziri Mhandisi Stella Manyanya na Naibu katibu Mkuu Dkt. Leonard Akwilapo, wakati kamati hiyo ilipofanya ziara ya kukagua mradi wa MLOGANZILA chuo kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS).








Jumapili, 19 Machi 2017

NAIBU WAZIRI AZINDUA VISHKWAMBI.

Naibu waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhandisi Stella Manyanya amewataka wadau wa Maendeleo ndani na nje ya nchi kuangazia maeneo ya vijijini kufuatia miradi mbalimbali ya maeneo kuangazia maeneo ya mijini zaidi.

Mheshimiwa Manyanya ametoa kauli hiyo hii leo katika shule ya msingi ya Olympio wakati akikabidhi vishkwambi (tablets)ambavyo vinatarajiwa kusambazwa katika shule mbalimbali za jijini Dar es salam.

Mhandisi Manyanya amesema umefika wakati sasa mradi wa majaribio kama huu wa Elimu kwa njia ya TEHAMA upelekwe hadi maeneo ya vijijini na siyo kubakia kwenye maeneo ya mijini pekee.

Naibu Waziri manyanya pia amewataka walimu kuhakikisha vifaa hivyo vinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa hasa ya kuwafundishia wanafunzi.