Ijumaa, 15 Februari 2019

SERIKALI YABAINISHA MIKAKATI YA KUZUIA MIMBA NA NDOA ZA UTOTONI

Serikali imesema inaendelea na mkakati wa kujenga mabweni katika shule mbalimbali za Sekondari hapa nchini ambazo ni za kutwa ili kuepusha watoto wa kike kupata mimba pamoja na kuzuia ndoa za utotoni.

Kauli ya Serikali imetolewa na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. William Ole Nasha wakati akifungua mkutano wa kimataifa wa kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa mradi wa Girls Inspire Tanzania wenye lengo la kuzuia ndoa za utotoni uliofanyika Jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe Wiliam Ole Nasha akizungumza na wadau wa Elimu (Hawapo pichani) wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kimataifa wa kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa mradi wa Girls Inspire Tanzania wenye lengo la kuzuia ndoa za utotoni Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri huyo amesema tatizo la ndoa za utotoni ni kubwa katika nchi nyingi hali ambayo inasababisha watoto wa kike kukosa haki yao ya msingi ya kupata elimu na kusababisha Taifa  kukosa wataalamu.

“Ndoa za utotoni zinafanya mtoto wa kike asisonge mbele katika safari yake ya elimu  na ndio maana serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali   kuhakikisha tunazuia ndoa za utotoni na kuweka mazingira wezeshi ya kuwafanya watoto wa kike waendelee kubaki shuleni kupata elimu,” alisema Mhe. Ole Nasha.
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Wiliam Ole Nasha na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi wa wadau wa elimu waliohudhuria mkutano wa mkutano wa kimataifa wa kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa mradi wa Girls Inspire Tanzania.

Akizungumza wakati wa kufungua mkutano huo Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema Wizara ya Afya na Wizara ya Elimu zinashirikiana kuhakikisha shule za msingi na sekondari zinakuwa na Walimu ambao watasaidia kutoa ushauri nasaha kwa wanafunzi kufahamu namna ya kujizuia kuingia katika  ndoa na mimba za utotoni.

Mradi wa Girls Inspire Tanzania una lenga kuzuia ndoa za utotoni unatekelezwa katika nchi za Tanzania, Msumbiji, Bangladesh, India na Pakistani na kufadhiliwa na na serikali za Canada na Australia ambapo kwa Tanzania umatekelezwa na Taasisi ya Elimu ya Watu wazima na Shirika lisolo la Serikali Kiota Women Health and Development, (KIHOWEDE).

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Wiliam Ole Nasha akiwa na  Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, Balozi wa Canada O’Donnell na Mwenyekiti wa Baraza la Usimamizi wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima Tanzania Dkt. Naomi Katunzi wakifuatilia uwasilishwaji wa mada wa katika mkutano wa kimataifa wa kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa mradi wa Girls Inspire Tanzania.

WAZIRI NDALICHAKO AAHIDI USHIRIKIANO MAANDALIZI YA ZANZIBAR JAMBO REE


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia ambaye pia ndiye  Rais wa Skauti Profesa Joyce Ndalichako amewaahidi ushirikiano Viongozi wa Chama cha Skauti Tanzania katika kufanya maandalizi ya sherehe za  Zanzibar Jambo Ree inayotarajiwa kufanyika mwezi wa sita mwaka huu Visiwani Zanzibar..

Waziri Ndalichako amesema hayo wakati alipokutana na kuzungumza na Viongozi wa  Juu wa Skauti Tanzania kwa lengo la kumuelezea  Waziri hatua iliyofikiwa katika maandalizi ya sherehe hizo.

Waziri Ndalichako amewaambia viongozi hao wa skauti kuwa ni vyema wakaliangalia kwa makini pendekezo lao la kutaka kupeleka washiriki 24 Visiwani Zanzibar kutoka kila mkoa wa Tanzania bara kwani namba hiyo itakuwa ni kubwa, na kuzifanya sherehe hizo kuonekana ni za Bara badala ya Zanzibar.


 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akizungumza na Skauti Mkuu Mwantumu Mahizi na Kamishana Mkuu Grace Joseph jijini Dar es salaam ambapo Waziri amewaahidi viongozi wa skauti ushirikiano katika maaandalizi ya Sherehe za Jambo Ree zinazotarajiwa kufanyika visiwani Zanzibar.



 “Ninawashauri kuangalia kwa undani na makini suala la idadi ya washiriki kutoka Bara kwa kila mkoa washiriki 24, idadi hii ni kubwa na tutawazidi kwa kuwa Zanzibar  ina mikoa michache kuliko sisi na sherehe hizi zitaonekana kuwa ni za Bara na si Zanzibar,” alisema Waziri.

Skauti Mkuu Mwantumu Mahiza alimwelezea Waziri kuwa Chama cha Skauti Tanzania kinatekeleza agizo la Makamu wa Rais alilolitoa wakati wa maadhimisho ya Siku ya Skauti Dunia na Maadhimisho ya miaka mia moja ya Skauti hapa nchini ya kukitaka chama hicho kufanya sherehe  hizo Visiwani Zanzibar.

Mahiza pia alimtambulisha Kamishna Mkuu mpya Grace Joseph Kado aliyeteuliwa hivi karibuni na kueleza kuwa sasa safu ya uongozi  kwa sasa imekamilika.
Skauti Mkuu Mwantumu Mahizi akisisitiza jambo kwa Rais wa Skauti Tanzania ambaye pia ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako wakati wa kujadiliana kuhusu maandalizi ya sherehe za Jambo Ree zinazotarajiwa kufanyika visiwani Zanzibar.

Jumatano, 13 Februari 2019


UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY

STUDY OPPORTUNITY TENABLE IN THE REPUBLIC OF KOREA FOR ACADEMIC YEAR 2019-2021
1.0 Call for Application
The general Public is hereby informed that, the National Institute for International Education (NIIED) under the Ministry of Education of the Republic of Korea is offering Graduate study opportunity to a Tanzanian citizen for  the academic year 2019 Global Korea Scholarship: Korean Government Scholarship Program for International Students for a Graduate Degree (2019 Graduate GKS).

2.0 Mode of Application
All applicants are required to complete application form and attach all requested documents. Instructions for this Scholarship are obtained in the following website http://www.studyinkorea.go.kr.

Application forms and attached documents should be submitted to the Korean Embassy not later than 7th March, 2019
PHYSICAL ADDRESS
19TH Floor Golden Jubilee Tower,
Ohio Street, City Centre,
P. O. Box 1154,
DAR ES SALAAM.




Issued by
Permanent Secretary,
Ministry of Education, Science and Technology,
College of Business Studies and Law,
University of Dodoma (UDOM) Building No. 10,
P. O. Box 10,
40479 DODOMA.


UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY

STUDY OPPORTUNITY TENABLE IN THE THAILAND FOR ACADEMIC YEAR 2019-2020
1.0 Call for Application
The general Public is hereby informed that, the Thailand International Cooperation Agency (TICA) announces scholarships for Master’s degree under the Thailand International Postgraduate Programme (TIPP) for the academic year 2019.

2.0 Mode of Application
The application and the corresponding application documents should be submitted to application receiving agency, the Permanent Secretary, Ministry of Education, Science and Technology. For more information, please visit the following link: http://tica.thaigov.net/main/en/  and an application form is found in the following link: http://www.tica.thaigov.net/main/en/relation/75500-TIPP-Application-form.html

Eligibility criteria for candidates and required documents are as per the applied programme. For more information please visit the following link: http://tica.thaigov.net/main/en/relation/99237-TIPP-2019.html.

Note that: late or incomplete applications/documents will not be considered.

Deadline for receiving application forms is on 15th March, 2019.


Issued by
Permanent Secretary,
Ministry of Education, Science and Technology,
College of Business Studies and Law,
University of Dodoma (UDOM) Building No. 10,
P. O. Box 10,
40479 DODOMA.


THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY


Tender No. ME-024/2018-19/HQ/G/05


For

SUPPLY OF SPECIAL NEEDS MATERIALS (TESP)

Invitation for Tender

Date: 13th February, 2019
1.       This Invitation for Tenders follows the General Procurement Notice (GPN) which appeared on PPRA website online on 02nd October, 2018.

2.       The Ministry of Education, Science & Technology has received a grant from the Global Affairs Canada (GAC) towards the cost of Teacher Education Support Project, and it intends to apply part of the proceeds of this grant to cover eligible payments under the contract for Supply of Special Needs Materials.

3.       Tendering will be conducted through the National Competitive Tendering procedures specified in the Public Procurement Regulations, 2013 – Government Notice No. 446 as amended in 2016 and are open to all Tenderers as defined in the Regulations.
4.       Interested eligible Tenders may obtain further information from and inspect the Tendering Documents at the office of the Secretary of Tender Board, Ministry of Education, Science & Technology, College of Business Studies and Law, Universities of Dodoma, (UDOM), Block 10, P.O Box 1040479Dodoma, Office number 320 from 0900 to 1500 hours on Mondays to Fridays inclusive except on public holidays.

5.       A complete set of Tendering Document (s) in English and additional sets may be   purchased by interested Tenderers on the submission of a written application to the address given under paragraph 4 above and upon payment of a non-refundable fee of Tzs. 100,000/= (Tanzania Shillings: One hundred Thousand Only), Payment should be done through Government e-Payment Gateway (Gepg) where the tenderer should get Control number at Ministry of Education, Science and Technology, Room No. 327.

6.       All Tenders must be accompanied by a Tender Security in an acceptable form in the amount of TZS. 5,000,000.00 (Tanzanian shillings Five million) be in the form of a Bank Guarantee in the format provided in section IX.

7.       All tenders in one original plus two copies properly filled in, and enclosed in plain envelopes must be delivered to the Secretary of Tender Board, Ministry of Education, Science & Technology, College of Business Studies and Law, Universities of Dodoma, (UDOM), Block 10, P.O Box 10 - 40479Dodoma, Room 320 at or before 10:30HRS, on 22nd February, 2019. Tenders will be opened at 10:45 hrs in public and in the presence of Tenderers’ representatives who choose to attend in the opening at the Conference Room, Ground Floor, Ministry of Education, Science & Technology, College of Business Studies and Law, Universities of Dodoma, (UDOM), Block 10, P.O Box 10 40479Dodoma.

8.       Late Tenders, Portion of Tenders, Electronic Tenders, Tenders not received, Tenders not opened and not read out in public at the tender opening ceremony shall not be accepted for evaluation irrespective of the circumstances.


PERMANENT SECRETARY,
MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE & TECHNOLOGY
University of Dodoma (UDOM), Block No. 10, P.O. Box 10   40479 DODOMA.


WAZIRI NDALICHAKO AAGIZA KUSIMAMISHWA KAZI ALIYEKUWA MKUU WA CHUO CHA UALIMU ILONGO NA WATUMISHI WENGINE WAWILI


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Leonard Akwilapo kumvua madaraka na kumsimamisha kazi Benjamini Mwilapwa aliyekuwa Mkuu wa Chuo cha Ualimu Ilonga kabla ya kuhamishiwa Chuo cha Ualimu Mpwapwa  kwa kushindwa kusimamia ukarabati  Chuoni hapo.

Waziri Ndalichako pia amemuagiza Dkt. Akwilapo kuwasimamisha kazi watumishi wengine akiwemo afisa manunuzi na ugavi Ally Masanja na Muhasibu Godlove Yona ambao ni watumishi wa chuo hicho ili kupisha uchunguzi kwa kile kinachodaiwa kufanya manunuzi yasiyofuata taratibu na kulipa fedha kwa kazi ambazo hazijakamilika.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akikagua miundombinu ya ujenzi wa mabweni katika Chuo cha Ualimu Ilonga kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro.

Waziri Ndalichako ametoa maagizo hayo  mkoani Morogoro  alipofanya ziara chuoni hapo ya kukagua maendeleo ya ujenzi, na uboreshaji wa miundombinu inayofanywa na Wizara hiyo.

Amesema ukarabati uliofanyika hauridhishi huku aliyekuwa Mkuu wa Chuo hicho ambae ndie  alikuwa mwenyekiti wa kamati za ujenzi na manunuzi  chuoni hapo kuwa  mtoa maamuzi ya mwisho bila kujali kufuata  sheria ya manunuzi inayoelekeza unapotumia Force Akaunti unatakiwa kuwa na kamati aina gani na majukumu yake ni yapi. 

“Inaonekana Mkuu wa Chuo alipora madaraka, ninafahamu kuwa amehamishiwa Chuo cha Ualimu Mpwampwa  sasa namuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia amrudishe na avuliwe madaraka mara moja, haiwezekani mtu akapandishwa cheo wakati Chuo hiki ambacho ni kidogo kilimshinda kusimamia ukarabati”, alisisitiza Waziri Ndalichako.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akiangalia sakafu ya moja ya bweni lililokarabatiwa lakini bado imeonesha kuchakaa kwa muda mfupi.

Aliongeza kuwa kazi zilizofanyika za ukarabati chuoni hapo niza ubabaishaji na kwamba zimefanyika chini ya kiwango, akitolea mfano sakafu kwenye majengo yote kuonesha nyufa, huku nyongeza ya gharama za ukarabati zikiwa kubwa.

Pia Waziri Ndalichako amemtaka Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST) Profesa Joseph Msambichaka kufika katika Chuo Cha Ualimu Ilonga  siku ya  kesho , February 13, 2019 kuona namna wataalamu wa taasisi hiyo  walivyoshindwa kusimamia kazi waliyokabidhiwa kwao ambao ni  washauri elekezi.

Pia amemtaka Katibu Mkuu kuvisimamia kwa karibu vyuo vya ualimu kwa  kuwa sasa vimeanza kuwa kama vichaka ambapo michango haifuati utaratibu ikiwa  ni pamoja na kuitaka timu  ya wakaguzi wa wizara  waliofika chuoni hapo kufanya uchunguzi wa kina   kwa sababu inaelekea kuna mahali pengine nyaraka zilikuwa zinaghushiwa.
Muonekano wa Jengo la Utawala lililokarabatiwa katika Chuo cha Ualimu Ilonga kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi ameiomba wizara kama iliyo katika miradi  mingine inayotekelezwa na Serikali katika Wilaya hiyo kuhakikisha wanawahirikishwa kwa karibu ili waweze kusimamia kile kinachotekelezwa katika eneo husika.
Zaidi ya Shilingi bilioni moja zimetolewa na Serikali kukarabati Chuo cha Ualimu Ilonga kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, mkoani Morogoro.

Jumatatu, 11 Februari 2019


UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY

STUDY OPPORTUNITY TENABLE IN THE UNITED STATE OF AMERICA FOR ACADEMIC YEAR 2019

1.0 Call for Application
The general Public is hereby informed that, the United States Embassy Public Affairs’ Section  is now accepting application for 2020 Fulbright Foreign Student Programme  to pursue Master`s and Doctorates Degrees offered in the US Universities for the academic year 2019.

U.S. Embassy encourages candidates with disabilities to apply as special accommodations are available.

2.0 Mode of Application
Applications must be submitted online using the Embark Visiting Scholar system, accessible at https://apply.iie.org/ffsp2020The submission deadline for applications is April 5, 2019. For more information, please email drs_exchanges@state.gov.

Issued by
Permanent Secretary,
Ministry of Education, Science and Technology,
College of Business Studies and Law,
Universities of Dodoma (UDOM) Building No. 10,
P. O. Box 10,
40479 DODOMA.