Jumatano, 10 Aprili 2019



UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
MINISTRY OF EDUCATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY


SCHOLARSHIP TENABLE IN THE GOVERNMENT OF INDONESIA 2019-2020
 
Call for Application
The General Public is hereby informed that, the Kemitraan Negara Bekembang (KNB), offers scholarship opportunity to Tanzanian to study different programme in various University in Indonesia.

Mode of Application
All interested candidates should apply through an online application found in the following link: http://www.knb.ristekdikti.go.id/ .

Furthermore, information visit the following links: file:///E:/KNB_Application_Guidelines_2019.pdfand http://www.knb.dikti.go.id/
Other require documents
Recommendation letter is issued by the Embassy and is mandatory; it can be required by submitting the required documents (invitation letter, Passport or birth certificate, academic certificates and academic transcript) to the Embassy of the Republic of Indonesia or via email: zefanyatodoan@gmail.com
The online application should be completed no later than April 12th, 2019
Issued by:
Permanent Secretary,
Ministry of Education, Science and Technology,
University of Dodoma,
College of Business and Law,
Block 10,
P .O. Box 10,
40479 Dodoma.

Jumatatu, 8 Aprili 2019

NORWAY NA TANZANIA KUENDELEA KUSHIRIKIANA KATIKA SEKTA YA ELIMU


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Norway nchini Tanzania Elisabeth Jacobsen mjini Dodoma ambapo pamoja na mambo mengine wamezungumzia kuendeleza ushirikiano katika sekta ya elimu kati ya nchi hizo mbili.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akifanya mazungumzo na Balozi wa Norway Elisabeth Jacobsen kuhusu Sekta ya Elimu.

Waziri Ndalichako ameishukuru serikali ya Norway kwa kuendelea kufadhili sekta ya elimu kupitia Mfuko wa Global Partnership for Education (GPE ) na amemuhakikishia Balozi Jacobsen kuwa fedha zote zinazotolewa na kupitia mpango huo zitatumika kama ilivyokusudiwa.

Waziri Ndalichako amevitaja vipaumbele vya ufadhili huo kuwa ni masuala ya uthibiti ubora wa shule, ununuzi wa  vitabu na kutoa  mafunzo kwa walimu walio kazini.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Norway Elisabeth Jacobsen pamoja na viongozi wengine Mjini Dodoma

Kwa upande wake Balozi wa Norway nchini Tanzania, Elisabeth Jacobsen, ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa kupiga hatua kubwa katika elimu na kueleza kuwa wanaridhishwa na utekelezaji wa mradi wa uanzishaji Kituo cha kufuatilia Hewa ya Ukaa katika  Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA).

Kituo hicho kinafadhiliwa na Serikali ya Nchi ya Norway kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akiagana na Balozi wa Norway Elisabeth Jacobsen

Jumatatu, 1 Aprili 2019

WAZIRI WA ELIMU AZINDUA UKUMBI WA KISASA WA MIHADHARA CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE


Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amezindua ukumbi wa mihadhara wa kisasa katika Chuo Cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere uliojengwa mapato ya ndani ya Chuo hicho.

Akizundua ukumbi huo wa Mihadhara kigamboni jijini Dar es salaam Waziri Ndalichako amepongeza Bodi ya Utawala na Uongozi wa Chuo hicho kwa kusimamia vema matumizi ya fedha zinazotokana na Mapato ya ndani na kutumia kutekeleza miradi yenye tija kwa Chuo na Taifa kama ilivyofanyika katika ujenzi wa Ukumbi huo na pia amewataka uongozi kusimamia Dira na Dhima ya uanzishwaji wake kwa kujikita katika kutoa mafunzo ya Uongozi, Utawala na Maadili.

Waziri Ndalichako amewapongeza Watendaji wa Chuo kwa kusimamia kwa karibu utekelezaji wa Mradi huo hadi kufikia hatua ya kukamilisha japo kwa kuchelewa kwa karibu miezi tisa.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akikata utepe kuashiria  uzinduzi wa Ukumbi mpya wa Mihadhara uliyojengwa katika Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Kampasi ya Kivukoni uliojengwa kwa kutumia mapato ya ndani ya Chuo hicho.

“ nimefurahishwa na kazi hii nzuri iliyofanyika hapa, kwakweli ni jengo zuri lenye ubora wa hali ya juu na ambalo litawafanya wanafunzi kuongeza ari ya kujifunza na ninategemea kuona jengo hili likituzwa vizuri ili litumike kwa miaka mingi likiwa na ubora uleule”. Amesisitiza Ndalichako

Aidha Ndalichako amezitaka Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kuthamini na kutumia vizuri mapato yake ya ndani kwa ajili ya kutekeleza mipango na Miradi mbalimbali ya Maendeleo katika taasisi hizo ili kuleta maendeleo ya haraka badala ya kuzitumia fedha hizo kwa matumizi mengine yasiyo na tija.

Wakati huo amewataka Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) ambao ni wakandarasi  wa ujenzi wa Ukumbi huo kukamilisha miradi mingine iliyo chini ya Wizara ya Elimu ikiwemo ukarabati wa shule Kongwe mfano Kibaha Sekondari, Shule ya Sekondari ya Wasichana Songea pamoja na ujenzi wa Hosteli na miundombinu mingine katika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili Kampasi ya Mloganzila.

 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akimpongeza Mwenyekiti wa Bodi ya Utawala wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyereer Stepen Wasira wakati wa uzinduzi wa Ukumbi wa Mihadhara uliyojengwa katika Chuo hicho.



Nae Mwenyekiti wa Bodi ya Utawala ya Chuo hicho Stephen Wasira, amesema Chuo hicho kimejipanga kuhahakisha kinatoa elimu bora na wahitimu walio bora wenye weledi hasa katika eneo la uongozi na utawala ili kuenzi fikra na maono ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alieanzisha chuo hicho Mwaka 1961 kwa lengo la kuandaa viongozi na watawala.

Awali, Mkuu wa Chuo Prof. Shadrack Mwakalila akitoa taarifa ya mradi amesema jengo hilo limegharimu zaidi ya Shilingi za Tanzania Bilioni 1.1  na kwamba lina uwezo wa kuchukua wanafunzi 330 kwa wakati mmoja. Ameongeza kuwa pamoja na ukumbi wa Mihadhara jengo hilo lina ofisi nane za wahadhiri na mifumo ya kisasa ya sauti.
 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akisalimiana na Bibi Thabita Siwale Waziri wa kwanza wa Elimu mwanamke Tanzania ambae pia alipitia mafunzo katika Chuo hicho aliyehudhuria hafla ya uzinduzi wa Ukumbi wa Mihadhara uliyojengwa katika Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.




Jumapili, 31 Machi 2019

WIZARA YA ELIMU KUJENGA MAABARA YA FIZIKIA KATIKA SHULE MAALUM YA WASICHANA KISARAWE


Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia  kujenga maabara ya Fizikia  katika shule mpya maalum ya wasichana inayotarajiwa kujengwa katika wilaya ya Kisarawe.

Ahadi hiyo imetolewa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya uchangiaji fedha kwa ajili ya kujenga shule hiyo ambapo Waziri Ndalichako amesema pamoja na kujenga Maabara pia itatoa vifaa vyote vya maabara hiyo lengo likiwa kuhamasisha na kuongeza fursa za watoto wa kike kisarawe na kwingine nchini kusoma masomo ya sayansi.

Akizungumzia hafla ya kuchangia fedha kwa ajili ya kujenga shule hiyo maalum Waziri Ndalichako ameipongeza wilaya ya Kisarawe kwa kuja na kampeni ya Tokomeza Zero yenye lengo la kuboresha elimu katika wilaya hiyo huku mkazo ukiwekwa katika  kumuondolea mtoto wa kike changamoto anazokabiliana nazo wakati wa kujifunza kwa kuhakikisha anapata mazingira rafiki na salama ya kujifunzia.
 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Joyce Ndalichako akizungumza na wadau mbalimbali wa elimu (hawapo pichani) walioitikiwa wito wa kuchangia ujenzi wa shule maalum kwa ajili ya watoto wa kike katika Wilaya ya Kisarawe



“Mtoto wa kike anapokuwa anatembea umbali mrefu kutoka shuleni kwenda nyumbani njiani anakutana na majaribu na vishawishi vingi vinavyokwamisha lengo lake la kupata elimu, kwa hiyo kuamua kujenga shule maalum kwa ajili ya mtoto wa kike ni uamuzi mzuri kwani  itawapa fursa kuweza kukaa na kusoma vizuri zaidi na hii ni hatua kubwa sana katika kuunga mkono Jitihada zinazofanywa na Rais wetu” Amesema Ndalichako.

Ndalichako amesemea  tathimini inaonyesha ufaulu kwa ujumla kwa mtoto wa kike uko chini ukilinganisha na watoto wa kiume kwa hiyo ujio wa shule hii maalum kwa ajili ya mtoto wa kike ni muhimu kutokana na mazingira wanayoishi ambapo wanaporudi kutoka shule wanakuwa na majukumu mengi ya nyumbani na kuwanyima muda wa kujisomea.

Naye Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Suleiman Jafo amesema wilaya ya Kisarawe imeweka mikakati mbalimbali ya kuhakikisha inapunguza ziro na kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia ikiwemo kuondoa changamoto ambazo zimekuwa zikikwamisha wanafunzi kujifunza hasa kwa mtoto wa kike.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Joyce Ndalichako, Waziri wa Maliasili na Utalii na Mbunge wa Viti maalum wa Kisarawe Zainabu Vulu wakifatilia kwa makini zoezi la  wa kuchangia ujenzi wa shule maalum kwa ajili ya watoto wa kike katika Wilaya ya Kisarawe

“Wilaya ya Kisarawe imekuwa na utaratibu wa kufanya tathimini kila matokeo yanapotoka ili kuona nafasi ya wilaya katika ufaulu na kuziangalia changamoto ambazo zinakwamisha faulu na kuziwekea mikakati ili kuboresha mazingira ya kfundishia na kujifunza ” amesema Waziri Jafo.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Joketi Mwegelo alimweleza Waziri wa Elimu kuwa lengo la kuanzishwa kwa Kampeni ya Tokomeza Zero ni kuongeza na kuboresha miundombinu ya shule ili kuifanya kuwa rafiki na salama kwa utoaji wa elimu.

Mwegelo amesema ujenzi wa shule maalum katika wilaya ya kisarawe  ya uchangia ni moja ya mkakati mahsusi wa kukabiliana na changamoto zinazowakabili watoto wa kike ili kuwawezesha kupata muda wa ziada wa kujifunza zaidi.

Shule ya Sekondari maalum inayotarajiwa kujengwa katika wilaya Kisarawe itachukua wanafunzia wa kidato cha kwanza mpaka cha sita na inakadiriwa kugharimu zaidi ya shilingi bilioni moja na nusu ambazo zinahusisha ujenzi wa miundombinu ya mabweni, madarasa, maabara, matundu ya vyoo pamoja na nyumba za walimu.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Joyce Ndalichako na  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Suleiman Jafo kwa pamoja wakipokea mfano wa hundi ya shilingi milioni kmi iliyolewa na kampuni ya star times kwa ajili ya ujenzi wa wa shule maalum kwa ajili ya watoto wa kike katika Wilaya ya Kisarawe