Jumanne, 6 Desemba 2016

Waziri wa Elimu hakutana na Ujumbe wa Benki ya Dunia



Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akiongea na wajumbe kutoka Benki ya Dunia waliofika wizarani kuongea naye masuala mbalimbali ya Elimu na jinsi ya benki hiyo itakavyoendelea kusaidia sekta ya elimu nchini wengine katika picha ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo, Sajitha Bashir, Cornelia Jesse na Gayle Martin kutoka Benki ya Dunia.
Katika mazungumzo hayo, Waziri wa Elimu aliishukuru Benki ya Dunia kwa kuendelea kushiriki katika miradi mbalimbali ya elimu ambayo imekuwa chachu ya kuleta maboresho katika sekta ya elimu nchini. Hivyo amewaomba kuendelea kusaidia kutoa misaada mbalimbali katika elimu ili kuhakikisha inaendelea kuboreshwa na kuwapa fursa watoto waengi wa Kitanzania kupata elimu iliyo bora.
Naye Mjumbe kutoka Benki ya Dunia Sajitha Bashir amemuhakikishia Waziri wa Elimu kuwa Benki ya Dunia itaendelea kufadhili miradi ya Elimu nchini pale itakapoitajika. Aidha, alisisitiza kuwa miradi yote inayofadhiliwa na Benki ya Dunia ni lazima itoe matokeo yanayokusudiwa

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni