Jumanne, 26 Septemba 2017

TATHMINI YA MWAKA 2016, P4R

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na OR - TAMISEMI kwa kushirikiana na Washirika  wa maendeleo leo wamekutana mjini Dodoma kufanya Tathmini  ya utekelezaji wa Programu ya Lipa Kulingana na Matokeo ( EP4R)  kwa mwaka 2016/17 ili kuona mafanikio yaliyopatikana, changamoto na kuweka mikakati ya kutatua changamoto zilizopo katika suala la utoaji wa Elimu bora Nchini.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo Mratibu wa Programu ya Lipa Kulingana na Matokeo  Gerald Mweli kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia amesema programu hiyo inafanya tathmini ili kujua hali halisi ya utekelezaji wa majukumu, kwa kiasi gani mradi umefanikiwa lakini pia kuona changamoto na namna ambavyo serikali kwa kushirikiana na washirika wa watakavyozitatua.

Mweli ametaja  mafanikio yaliyopatikana kupitia mradi huo,kuwa ni pamoja na  kujenga na kukarabati  miundombinu chakavu ya shule za Msingi na Sekondari zipatazo 361 kutoka katika Halmashauri 129, vyumba vya mdarasa 1,435, mabweni 261, majengo ya utawala 11, mabwalo 4, vyoo 2,832, nyumba za walimu 12, maktaba 4, na uwekaji wa maji katika shule nne (4).

Kwa upande wa vyuo vya ualimu programu imefanikiwa kukarabati  vyuo 10 vya ualimu ikiwa ni pamoja na kununua  compyuta 260 zitakazowawezesha walimu  kutekeleza  majukumu yao kwa urahisi, magodoro 6,730 yatakayotumiwa na wanafunzi pamoja na viti 1976 kwa ajili ya wanachuo.


Aidha, programu imenunua vifaa vya maabara 1,696 kwa ajili ya shule za sekondari ambavyo zitasaidia katika ufundishaji wa masomo ya sayansi na kuongeza uelewa kwa wanafunzi.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni