Alhamisi, 16 Novemba 2017

Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii yakagua Shule ya Ihumwa

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya huduma za maendeleo ya jamii imepongeza juhudi zinazofanywa na Wizara ya Elimu, Sanyasi na Teknolojia kwa kushirikiana na OR TAMISEMI katika kuboresha miundombinu ya shule, ikiwa ni pamoja na kusimamia fedha zinazotengwa kwa ajili ya uboreshaji wa miundombinu hiyo.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Peter Serukamba wakati kamati hiyo ilipotembelea na kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa 9, matundu ya vyoo na jengo la Utawala katika shule ya msingi Ihumwa ujenzi ambao umetekelezwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia programu ya Lipa kulingana na Matokeo, yaani P4R.
Ziara hiyo imejionea madarasa mapya 9, ukarabati wa vyumba vya madarasa 11, Jengo la utawala na ujenzi wa vyoo ambavyo vyoye vimegharimu milioni 168.

Mwenyekiti wa kamati hiyo pia amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu kutoa fedha kwa ajili ya kuchimba kisima katika shule ili kuondoa adha ya upatikanaji wa maji katika shule hiyo.

Kwa upande wake Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia amemhakikishia Mwenyekiti wa kamati hiyo kuwa Wizara imepokea maelekezo na kuahidi kuyafanyia kazi.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni