Jumanne, 5 Desemba 2017

Vijana watakiwa kuwa na hofu ya Mungu.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako amesema  Mipango ya Taifa haliwezi kufanikiwa bila kuwa na vijana waadilifu,wachapakazi na wenye hofu ya mungu  hivyo amewataka vijana kuzingatia masomo ili kuweza kufikia malengo yanayikusudiwa Katika Taifa.

Waziri Ndalichako amesema hayo mwishoni mwa wiki wakati wa ibada maalumu iliyifanyika katika kanisa la City Christian Center lililopo Upanga Jijini Dar es Salaam ambapo amesema ili mtu yeyote afanikiwe katika maisha lazima hofu ya mungu iwepo katika maisha ya kila siku.

Waziri Ndalichako amesema vijana wengi wamekuwa wakitumia muda wao mwingi kufanya mambo ambayo siyo msingi wa maisha kama vile kujiingiza  kwenye makundi ya utumiaji wa dawa za kulevya, uporaji, unywaji wa pombe vitendo ambavyo havina faida na matokeo yake ni kijana kuangamia.

Kwa upande wake Askofu Mkuu wa Kanisa hilo la City Christian City Dkt. Reinwell Mwenisongole amepongeza juhudi zinazofanywa na serikali UA awamu ya Tano katika kusimamia Elimu ikiwa ni pamoja na kuongeza udahili katika vyuo vikuu, kujenga na kuboresha miundombinu ya vyuo vikuu kwa lengo la kusaidia kuongeza wataalamu ili kutimiza azma ya serikali ya kufikia uchumi wa viwanda.

Askofu Mwenisongole amesema kanisa la kanisa la Christian Center lilianzishwa mwaka 1978 kwa lengo la kuwasaidia vijana kuwa na hofu ya mungu.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni