Ijumaa, 11 Mei 2018

NAIBU WAZIRI OLE NASHA: LESENI ZA BIASHARA SI KIGEZO CHA MWANAFUNZI KUPATA MKOPO ELIMU YA JUU.



Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha amesema kumiliki biashara au kuwa na leseni ya biashara si kigezo cha kuamua kama mwanafunzi anastahili kupata mkopo au asipate mkopo

Naibu Waziri Ole Nasha ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari mijini Dodoma kufuatia taarifa ambazo zimesambaa kwenye vyombo mbalimbali pamoja na mitandao ya kijamii zikieleza kuwa wafanyabiashara wenye leseni watoto wao hawatapata mikopo kwa ajili ya Elimu ya Juu.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani mjini Dodoma kutolea ufafanuzi kuhusu vigezo vinavyotumika katika  kutoa Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu. 

Amesisitizama kinachoangaliwa ni kipato ambacho mzazi au mlezi anakipata katika kazi anayoifanya kama kinaweza kumgharamia mtoto wake masomo ya Elimu ya Juu na sio kazi anayoifanya.
Naibu Waziri Ole Nasha amewataka wananchi kupuuza taarifa hizo za uongo na upotoshaji zenye lengo la kuvuruga utaratibu uliopo wa utoaji mikopo kwa wanafunzi wa Elimu ya Juu.
Waandishi wa Habari wakimsikiliza Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. William Ole Nasha wakati akitolea ufafanuzi kuhusu vigezo vinavyotumika kutoa Mkopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu leo Mjini Dodoma.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni