Jumatano, 9 Mei 2018

DK. SEMAKAFU AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA UNICEF


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Ave Maria Semakafu leo amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka UNICEF kwa lengo la kujengeana uelewa wa pamoja juu ya kile wanachokitekeleza kuhusuiana na Sekta ya Elimu.

Mazungunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Wizara Jijini Dodoma ambapo wote kwa pamoja wamekubaliana kuimarisha mawasiliano ili kuwezesha utekelezaji wa majukumu katika sekta hiyo.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Avemaria Semakafu akisisitiza jambo wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Timu ya Ujumbe kutoka UNICEF juu ya namna bora ya kutekeleza majukumu ya kielimu katika Sekta hiyo.

Shirika la Kimataifa la kuhudumia watoto UNICEF wanatekeleza shughuli za kielimu katika mikoa ya Mbeya, Iringa, Njombe, Songea, Kigoma na Tabora kwa kutoa mafunzo kwa waratibu Elimu Kata, mafunzo kwa walimu kazini kuhusu Elimu Jumuishi, lishe, uongozi na utawala kwenye Elimu. 


Kikao hicho pia kimejumuisha wajumbe kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI). 
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Avemaria Semakafu na Timu ya Ujumbe kutoka UNICEF, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) wakiwa katika mazungumzo ya namna bora ya kutekeleza shughuli za kielimu za Sekta hiyo.





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni