Jumatano, 4 Julai 2018

WAZIRI NDALICHAKO AIELEKEZA COSTECH KUPELEKEA MIONGOZO YA KUSAIDIA WABUNIFU KWENYE HALMASHAURI

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce NDALICHAKO ameitaka Tume ya Taifa ya Sayansi naTeknolojia, COSTECH -kuhakikisha miongozo yote ya namna yakuwasaidia wabunifu inapelekwa  katika ngazi ya Halmashauri ili kuwezesha kupatikana kwa bunifu zitakazosaidia nchi kufikia uchumi wa viwanda.

Waziri Ndalichako ametoa agizo hilo katika kongamano la  sita la Kitaifa la Sayansi, Teknolojia na ubunifu linalofanyika jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akizungumza na wanasayansi na wavunifu katika kongamano la sita la Kitaifa la Sayansi, Teknolojia na Ubunifu linalofanyika jijini Dar es Salaam.

Ndalichako amesema miongozo ikipelekwa kwenye halmashauri itasaidia  kupatikana kwa wabunifu watakaoendeleza  Teknolojia  na kufanya kazi katika viwanda.

Waziri huyo mwenye dhamana ya kusimamia Elimu, Sayansi na Teknlojia amesema uchumi wa viwanda unategemea Sayansi  na wataalamu wenye ujuzi wakutengeneza na kubuni bidhaa mbalimbali zitakazotumika   viwandani lakini pia kuiletea jamii Maendeleo.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akipata maelezo kutoka kwa Mwanafunzi wa Shule ya St Jude Erick Laizer kuhusu ubunifu wa mtambo wa ulinzi dhidi ya moto na wizi.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa COSTECH  Dkt. Amos Nungu, amesema Kongamano hilo la siku tatu Lina lengo la  kuimarisha kasi ya ukuaji wa uchumi, ikiwa ni pamoja  na kuanzisha na kuendeleza viwanda.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akizungumza na Abubakari Amani mtaalam aliyetengeza mashine ya kupurura ama kupura maharage katika   kongamano la sita la  Kitaifa la Sayansi, Teknolojia na Ubunifu linaloendelea jijini Dar es Salaam.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni