Ijumaa, 6 Julai 2018

DK. SEMAKAFU ASEMA HAKUNA ATAKAESALIMIKA MATUMIZI YA FORCE AKAUNTI


Serikali imesema haitasita kuchukua hatua za kisheria kwa mtu yeyote atakayekiuka utaratibu wa kutumia Force Akaunti katika kutekeleza shughuli za ujenzi na ukarabati kwenye Vyuo vya Maendeleo ya wananchi (FDC’S).

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknoloji Dk. Avemaria Semakafu  mjini Morogoro wakati wa akifunga mafunzo ya siku tatu kwa wakuu wa vyuo, maboharia na wahasibu kuhusu utaratibu wa kutumia Force Akaunti katika shughuli za ujenzi na ukarabati katika vyuo vya FDCs.
kuwa upo kisheria na kwa yeyote atakaepindisha utaratibu huo atawajibika kwa hilo. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Avemaria Semakafu akizungumza na wajumbe (hawapo pichani) wakati akifunga mafunzo ya matumizi ya utaratibu wa Force Account Mjini Morogoro. Amewataka wajumbe kuhakikisha wanafuata utaratibu huo.
Alisema utaratibu huo uko kisheria na kwamba mafunzo hayo yamelenga kuwawezesha kupata taaluma ya kutumia utaratibu huo  ambapo amewataka washiriki hao kwenda kutumia taaluma hiyo kama nyenzo kuleta mabadiliko wakati wa kutekeleza miradi katika maeneo yao.


 “Ni muhimu kwa Wakuu wa Vyuo na wote mtakaohusika katika shughuli za ujenzi na ukarabati kuhakikisha mnafuata sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa kwa kuwa hakuna atakaesalimika kwa kuvunja sheria hizi,” alisisitiza Naibu Katibu Mkuu huyo  Dk Semakafu.


Wajumbe wa Kikao wakifuatilia hotuba ya Naibu Katibu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Avemaria Semakafu wakati wa kufunga mafunzo ya matumizi ya Force Account kwa Wakuu wa Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi, Maboharia na Wahasibu yaliyofanyika mjini Morogoro.
Amesema Vyuo vya maendeleo ya Wananchi vilianzishwa kwa malengo mahususi ikiwa ni pamoja na kutoa stadi na mafunzo kwa wananchi hivyo miradi hiyo ikikamilika kwa wakati vyuo vitaweza kutimiza malengo yake lakini pia thamani halisi ya matumizi ya fedha (Value for Money) za ujenzi na ukarabati zitaonekana.

Mafunzo hayo ya utaratibu wa kutumia Force Akaunti yameshirikisha wajumbe kutoka Vyuo vya maenedeleo ya wananchi 11 na yameendeshwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia chini ya  mradi wa Kukuza Ujuzi na Stadi za Ajira (ESPJ).
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Avemaria Semakafu akiwa katika picha ya pamoja  na baadhi ya Washiriki wa mafunzo ya namna ya kutumia force Akaunti yaliyofanyika Mjini Morogoro.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni