Alhamisi, 16 Agosti 2018

DK. SEMAKAFU: WATHIBITI UBORA NA MAAFISA ELIMU FANYENI UFUATILIAJI SHULENI


Naibu Katibu Mkuu Dk. Ave Maria Semakafu amewataka Maafisa Elimu na Wathibiti ubora kuhakikisha wanafanya ufuatiliaji na kutoa taarifa kwenye Mamlaka zinazohusika ili changamoto hizo ziweze kupatiwa ufumbuzi.

Dk. Semakafu ametoa kauli hiyo leo Wilaya Magu mkoani Mwanza wakati akishiriki zoezi la ufuatiliaji wa miradi inayofadhiliwa na washirika wa Maendeleo kuhusu ufundishaji na ujifunzaji AJESR.
Naibu Katibu Mkuu Dk. Ave Maria Semkafu akizungumza na timu ya ufuatiliaji wa Maendeleo ya ujifunzaji na ufundishaji shuleni (Hawapo Pichani), Wilayani Magu, mkoani Mwanza.

Dk. Semakafu amesema suala la ufuatiliaji kwa viongozi waliopewa Mamlaka ni la lazima kwani itasaidia zaidi kubaini changamoto lakini pia ni sehemu ya uwajibikaji katika kutimiza malengo ya Taifa.

“Viongozi ni lazima tuwajibike katika kushughulikia masuala ya wananchi na siyo kusubiri kiongozi wa juu aje atoe maelekezo ndiyo tuanze kukimbizana, mfano wewe mthibiti ubora wa shule, au Afisa Elimu unakagua shule zako? unatatua changamoto au unasubiri mpaka Mkurugenzi wa Halmashauri atoe maelekezo?” Alisisitiza Dk. Semakafu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu Lutengano Mwalwiba ameahidi kuendelea kufanyia kazi changamoto mbalimbali zilizopo katika Halmashauri hiyo ili Taifa liweze kusonga mbele.
Baadhi ya wajumbe wa timu ya ufuatiliaji wa miradi inayotekelezwa na washirika wa Maendeleo wakipokea taarifa kutoka kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu Lutengano Mwalwiba, Mkoani Mwanza.

Amesema hakuna jambo ambalo litaweza kuwa mbadala wa Elimu, Elimu ni kila kitu sasa ikivurugwa Elimu Taifa haliwezi kusonga mbele.

“Tukiwa na misingi mizuri ya Elimu lazima Taifa tutafanikiwa, changamoto zipo na ndiyo maana viongozi tupo kama changamoto zisingekuwepo basi hata viongozi tusingekuwepo,” alisisitiza Mkurugenzi huyo.
Naibu Katibu Mkuu Dk. Semakafu akipokelewa katika Kituo Cha Ufundi Ihushi kilichopo Wilayani Magu, mkoani Mwanza

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni