Jumapili, 5 Agosti 2018

NDALICHAKO ATAKA SHULE YA SEKONDARI MANGA DELTA KUPANDISHA TAALUMA


Waziri wa Elimu, Sayamsi na Teknolojia Prof.  Joyce Ndalichako amewataka walimu wa shule ya sekondari Manga Delta iliyoko wilayani Kibiti mkoani Pwani kuhakikisha wanawasaidia wanafunzi kimasomo ili taaluma katika shule hiyo iweze  kupanda.

Waziri Ndalichako ametoa agiza hilo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Shule hiyo ambapo amesema hajaridhishwa na mwenendo wa taaluma katika shule hiyo.

Amesema pamoja na serikali kuwekeza fedha nyingi katika kuboresha miundombinu ya shule hiyo bado imekuwa ikishuka kitaaluma mwaka hadi mwaka.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalich ako akizungumza na wanafunzi, walimu na wazaza wa shule ya Sekondari Manga Delta iliyoko wilayani Kibiti mkoani Pwani. Waziri Ndalichako amewataka walimu wa shule hiyo kuhakikisha wanawasaidia wanafunzi kimasomo ili taaluma katika shule hiyo iweze  kupanda.

 “Serikali imeshatoa zaidi ya shilingi milioni 256 kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa miundombinu ya vyumba vya madarasa na bweni juhudi hizi ziende sambamba na ufundishaji ili taaluma ipande”  Alisisitiza Ndalichako

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akikabidhi ufunguo wa pikipiki kwa mmoja wa Waratibu Elimu Kata ambapo amekabidhi Pikipiki kumi na sita katika mkutano wa hadhara uliofanyika wilayani Kibiti Mkoani Pani. Waziri Ndalichako amewataka Waratibu Elimu Kata hao kutumia Pikipiki hizo katika shughuli zitakazosaidia kuboresha Elimu.

Aliongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Tano kila mwezi imekuwa ikitoa kiasi cha silingi bilioni 20. 8 kugharamia Elimu bila malipo pamoja na kutoa shilingi laki mbili na nusu za posho ya madaraka kwa Wakuu wa Shule na Waratibu Elimu Kata hivyo amewataka kuwajibika ili kupandisha taaluma ya shule hiyo.

Waziri wa Elimu amehitimisha ziara yake ya siku mbili ya kikazi wilayani Kibiti mkoni Pwani kwa kukabidhi gari ya Idara ya Udhibiti Ubora kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya hiyo pamoja na pikipiki kumi na sita kwa Waratibu Elimu Kata.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akifungua gari kabla ya kumkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Kibiti Alvera Ndabagoye kwa ajili ya Idara ya Udhibiti Ubora ya wilaya hiyo. Waziri Ndalichako amewataka Wadhibiti ubora nchini kufanya kazi zao kwa weledi

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni