Jumapili, 5 Agosti 2018

SHULE YA MSINGI KIOMBONI KUJENGEWA MIUNDOMBINU MIPYA


Waziri wa Elimu, Sayamsi na Teknolojia Prof.  Joyce Ndalichako amehaidi kujenga na kuboresha miundombinu ya madarasa na matundu ya vyoo katika Shule ya Msingi ya Kiomboni ambayo miundombinu yake kwa sasa ni chakavu.  

Waziri Ndalichako ametoa ahadi hiyo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Shule hiyo iliyopo katika Kijiji cha Kiomboni Kata Salawe Wilayani Kibiti Mkoani Pwani.

Amesema kuwa shule hiyo pamoja na kuwa chakavu ina upungufu wa vyumba vya madarasa hvyo kupelekea hali ya ufundishaji na ujifunzaji kuwa ngumu.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akikaribishwa na baadhi ya viongozi na wananchi wa Kijiji wa Kiomboni Wilayani Kibiti mkoani Pwani alipowasili katika kijiji hicho ili kujionea changamoto zinazoikabili shule ya msingi ya Kiomboni. Waziri Ndalichako aliwahaidi wanakijiji hao kuwa serikali kupitia wizara yake watajenga miundombinu mipya katika shule hiyo

"Nimezinguka katika shule hii nimejionea kwa macho yangu jinsi miundombinu yake ilivyo kwenye hali mbaya na ninaahidi kuwa wizara yangu itafanya uboreshaji wa miundombinu hii ili mazingira ya kujifunzia yaweze kuwavutia watoto kupenda shule  " Aesema Ndalichako.

Waziri huyo amesema Serikali ya Awamu ya Tano imedhamilia kuboresha miundombinu ya Shule kwa kukarabati na kujenga mipya ili kuwezesha watoto kjifunza katika mazingira rafiki.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako pamoja na viongozi wa wilaya ya Kibiti wakikagua miundombinu ya madarasa na matundu ya vyoo  ya shule ya msingi kiomboni ambayo yamechakaa. Waziri huyo yupo wilayani Kibiti katika ziala ya kukagua miradi ya elimu inayotekelezwa na wizara ya elimu kupitia programu ya EP4R

Ndalichako amewahakikishia walimu wa shule hiyo pamoja na wanakijiji kuwa ujenzi na Ukarabati huo utafanyika mapema kabla ya mvua za masika hazijaanza.

Awali katika taarifa yake Mkuu wa shule Musa Mapange  alimweleza Waziri kuwa Shule hiyo haina vyoo imara kwani vilivyokuwepo vimeharibika na kufungwa na sasa watoto wanajisaidia katika vyoo vilivyotengenezwa kwa dharula.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako, Mbunge wa Kibiti Ali Ungando na Mkuu wa Wilaya hiyo Philiberto Sanga wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi wa shule  msingi kiomboni. Ndalichako  amewataka wanafunzi hao kusoma kwa bidii.

Waziri Ndalichako upo katika ziara ya siku mbili ya kikazi Wilayani Kibiti mkoani Pwaniku kagua miradi ya Elimu inayotekelezwa na wizara Kupitia Programu ya Lipa Kulingana na Matokeo (EP4R)


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni