Ijumaa, 3 Agosti 2018

SERIKALI KUONGEZA RASLIMALI WATU WENYE UJUZI STAHIKI KATIKA UCHUMI WA VIWANDA

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amesema nchi inahitaji rasilimali watu yenye ufahamu na ujuzi stahiki katika kujenga uchumi wa viwanda.

Akizungumza katika ufunguzi wa kongamano na maonesho ya Wahandisi wanawake wa Taasisi ya Wahandisi Jijini Dar es Salaam Ndalichako amesema Wizara yake imeweka mikakati mbalimbali ili kuhakikisha nchi inakuwa na rasilimali watu ya kutosha, wenye ujuzi utakaowawezesha kuchangia maendeleo ya Taifa.
 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akizungumza na wa washiriki wa Kongamano na Maonesho ya Wahandisi Wanawake wa Taasisi ya Wahandisi iliyofanyika Jijini Dar es Salaam. Amesisitiza Wahandisi hao kuweka katika vitendo tafiti zao ili kuwasaidia wananchi katika kutatua changamoto.


“Tunao mradi wa Mkakati wa Kukuza Staadi za Kazi (ESPJ unaotekeleza Mkakati wa Kujenga Ufahamu na Ujuzi katika maeneo muhimu ya kiuchumi kwa Taifa, miongoni mwa maeneo hayo ni kilimo na uongezaji wa thamani ya mazao ya kilimo; viwanda, usafirishaji, Tehama, nishati, ujenzi na maeneo ya utalii na huduma ambayo uhandisi una mchago mkubwa.” Amesisitiza Ndalichako

Aametoa wito kwa wahandisi hao kuhakikisha wanafanya jitihada zaidi ya kutafuta njia za kuendeleza matokeo ya tafiti wanazofanya na kuziweka katika vitendo ili ziweze kuchangia ipasavyo ukuaji wa sekta ya viwanda nchini. 
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akitoa zawadi kwa Mhandisi Mama Kinasha ambaye ni miongoni wa wahandisi wa wa kwanza kusajiliwa na Taasisi ya Waandisi wakati wa ufunguzi wa Kongamano na Maonesho ya Wahandisi Wanawake wa Taasisi ya Wahandisi iliyofanyika Jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wake Kaimu Msajili wa Wahandisi Patrick Balozi amesema katika kufanikisha azma ya kuwa na  uchumi wa viwanda ni muhimu kama Taifa kuongeza idadi ya Udahili kwa wanaunzi wa fani za uhandisi ikiwa ni pamoja na kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia yatakayowavutia wanafunzi kupenda masomo ya sayansi

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akisikiliza maelezo kutoka kwa mmoja wa washiriki wa maonesho ya ubunifu katika toa ufunguzi wa Kongamano na Maonesho ya Wahandisi Wanawake wa Taasisi ya Wahandisi iliyofanyika Jijini Dar es Salaam.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni