Jumatano, 8 Agosti 2018

WAZIRI NDALICHAKO AZINDUA BODI YA HUDUMA ZA MAKTABA


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako ameitaka Bodi mpya ya Huduma za Maktaba Tanzania kuhakikisha inaanzisha Maktaba za Wilaya ili kuwawezesha watanzania wengi kunufaika na Elimu na Maarifa yatokanayo na usomaji wa vitabu.

Waziri Ndalichako ametoa agizo hilo Jijini Dar es Salaam wakati akizindua Bodi hiyo na kusisitiza kuwa kuwepo kwa maktaba hizo kutaondoa changamoto ya wananchi kutembea umbali mrefu kufuata maktaba za mikoa.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akimkabidhi Mwenyekiti wa Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania Prof. Rwekaza Mkandala Sheria za Bodi hiyo. 

“Wananchi wanapenda kusoma vitabu sasa natoa rai kwenu Bodi mpya mshirikiane na Halmashauri za Wilaya, Miji na Manispaa kuanzisha Maktaba katika Wilaya zote, sisi kama Serikali tutaendelea kutoa ushirikiano kuhakikisha tunaimarisha utoaji wa huduma za maktaba nchini.” Alisisitiza Ndalichako.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akimkabidhi Mwenyekiti wa Baraza laUsimamizi la Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) Naomi Katunzi Sheria za Bodi hiyo. Ameiagiza Baraza hilo kuweka vigezo vitakavyotumika kutoa Elimu nje ya mfumo rasmi.
Katika hatua nyingine Waziri Ndalichako ametemblea Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima na kuzindua Baraza la Usimamizi la Taasisi hiyo ambapo amelitaka  baraza hilo kuboresha vigezo vinavyotumika kusajili vituo vinavyotoa Elimu ya sekondari nje ya mfumo rasmi pamoja na kusimamia ubora wa elimu inayotolewa.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akiongea na Watumishi wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (Hawapo Pichani) wakati wa uzinduzi wa Baraza la Taasisi hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni