Jumatano, 19 Septemba 2018

PROF MDOE AMESEMA TANZANIA IKO TAYARI KUSHIRIKIANA NA IAEA KATIKA KUENDELEZA MATUMIZI SALAMA YA NGUVU ZA NYUKLIA


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa James Mdoe ameongoza ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano Mkuu wa 62 wa kimataifa wa kuendeleza matumizi salama ya nguvu za nyuklia unaofanyika mjini Vienna nchini Austria.

Akizungumza katika mkutano huo mjini Vienna Profesa Mdoe ameishukuru IAEA kwa kuisaidia nchi ya Tanzania mashine ya kuchunguza na kutibu saratani ambayo inatumika katika hospitali ya Bugando iliyopo mkoani Mwanza na misaada ya kiufundi katika hospitali ya Saratani ya Ocean Road iliyopo jijini Dar es salama pamoja na misaada ya kuwasomesha  wataalam kwenye eneo la Teknolojia  ya nguvu za nyuklia. 
     
Naibu Katibu Mkuu Profesa James Mdoe akizungumza katika mkutano wa kimataifa unaofanyika mjini Vienna, nchini Austria kuhusu matumizi salama ya nyuklia.

Profesa Mdoe pia amekieleza kikao hicho cha kimataifa kuwa nchi ya Tanzania iko tayari  kushirikiana na IAEA katika kuendeleza matumizi salama ya nguvu ya nyuklia. 

Balozi wa kudumu kwenye Mashirika ya Umoja wa Mataifa mjini Geneva nchini Uswis James Msekele naye anashiriki mkutano huo.

Mkutano huo ulioanza Septemba 17 utahitimishwa Septemba 21, 2018 huko mjini Vienna nchini Austria.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni