Jumanne, 23 Oktoba 2018

UFAFANUZI WATOLEWA KUHUSU WANAFUNZI KUJIUNGA UDSM


ALIYOYAZUNGUMZA NAIBU MAKAMU MKUU WA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM PROF. BONAVENTURE RUTINWA KATIKA KIPINDI CHA JAMBO TANZANIA LEO TBC.

1. Wale wote waliiomba Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM) wakafutiwa udahili kwa sababu ya kuwa wengi zaidi (over capacity) wamerudishwa wote bila masharti yoyote.

2. Prof. Rutinwa ameeleza kuwa wale walioko Dar es Salaam waendelee kuchukua barua zao za udahili (admission letter) kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na wale walioko mbali na Dar es Salaam watazipokea barua zao kuanzia tarehe 27/10/2018 watakapofika kwa usaili. 

3. Wataalamu wa mifumo ya kompyuta wanaandaa utaratibu ili waliodahiliwa wapokee barua zao kwenye akaunti zao za udahili.

4. Wanafunzi ambao wamekosa code au wameshindwa kuingiza codes UDSM au vyuo vingine watapewa utaratibu wa kwenda chuo wanachokitaka.

5. Kutakua na dirisha la wale waliokosa nafasi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa sababu ya Program hizo kujaa wapate nafasi ya kuomba tena.

6.Serikali imeendelea kuboresha Miundombinu katika Chuo hicho ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi ya vyumba vya madarasa na maabara kwa hali ya juu na ya viwango kwa ajili ya kuhudumia wanafunzi ambao chuo hicho inataka kuwadahili.


7. Serikali pia inaendelea kukiwezesha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuongeza idadi ya Wahadhiri wabobevu ili kukidhi uhitaji.

8. Leo ilikuwa ni siku ya mwisho kufunga udahili lakini mara baada ya kufanya kikao na Mhe. Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako alielekeza kuongezwa kwa siku hizo ili kutoa fursa zaidi kwa wanafunzi.


9. Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kinamshukuru sana Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako kwa kusaidia kutatua changamoto iliyokuwepo katika udahili kwa UDSM.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni