Jumanne, 28 Mei 2019

MAONESHO YA KWANZA YA ELIMU YA UFUNDI NA MAFUNZO YAZINDULIWA DODOMA


Serikali imesema imetenga kiasi cha shilingi bilioni 18 kwa ajili ya kujenga Chuo cha Ufundi kipya katika makao makuu ya nchini, jijini Dodoma.

Kauli hiyo ya Serikali imetolewa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako wakati wa maonesho ya kwanza ya Elimu ya Ufundi na Mafunzo, mjini Dodoma.

Waziri Ndalichako amesema Serikali itaendelea kuimarisha vyuo vya kati, kuhuisha mitaala ili kuendana na Teknolojia, ambapo tayari serikali imetenga kiasi cha shilingi Bilioni 40 kwa ajili ya ujenzi wa vyuo vya ufundi Stadi nchini.


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akihutumia washiriki wa maonesho ya kwanza ya Elimu ya Ufundi na Mafunzo pamoja na wananchi wa jiji la Dodoma (Hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa Maonesho hayo.

Waziri amevitaka vyuo vyote vya ufundi nchini kuzingatia taratibu, kanuni na sheria katika kuendesha vyuo hivyo na yeyeote ambaye hatakidhi vigezo basi chuo hicho kitanyang’anywa ithibati.

“Zoezi la ukaguzi kwa vyuo vya Ufundi ni endelevu, hivyo vyuo ni lazima vizingatie taratibu, kanuni na  sheria , na chuo ambacho  hatakidhi vigezo kitanyang’anywa ithibati.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa baraza la Uongozi wa baraza la Taifa la Ufundi (NACTE), Prof. John Kondoro amesema vyuo vilivyoshiriki ni zaidi ya 100 ambapo washiriki watapata fursa ya kukuza ushirikiano miongoni mwao.


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akisikiliza maelezo ya  baadhi ya bidhaa zilizotengenezwa na wanafunzi kutoka moja ya chuo kinachoshiriki katika maonesho ya kwanza ya Elimu ya Ufundi na Mafunzo Jijini la Dodoma.

Prof.Kondoro amesema ndani ya miaka miwili serikali imesaidia kuweza kukaguliwa kwa vyuo vyote 500 vya ufundi vilivyopo nchini Jambo ambalo halikwahi kufanyika katika miaka ya nyuma.

Prof. Kandoro amesema maonesho hayo ni jukwa la kukutanisha wadau, kutangaza na kuona namna watu wanavyoweza kujiajiri na siyo kusubiria kuajiriwa.
Waziri wa Elimu, Sayannsi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akipata maelezo kuhusu gari linalotumia gesi lililobuniwa na wataalamu kutoka Chuo cha Ufundi Dar es Salaam (DIT) lililopo katika maonesho ya kwanza ya Elimu ya Ufundi na Mafunzo yanayofanyika  jiji la Dodoma.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni