Ijumaa, 31 Mei 2019

WAZIRI NDALICHAKO AKIPONGEZA CHUO KIKUU MZUMBE KWA USIMAMIZI MZURI WA UJENZI WA HOSTELI ZA WANAFUNZI


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako  amekipongeza Chuo Kikuu Mzumbe kwa usimamizi mzuri wa mradi wa ujenzi wa hosteli za wanafunzi unaoendelea Chuoni hapo.
Waziri Ndalichako ametoa pongezi hizo Mkoani Morogoro wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa hosteli za wanafunzi unaoendelea Chuoni hapo ambapo amesema ameridhishwa na kasi na ubora wa majengo yanayojengwa

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akiongozana na Viongozi pamoja na wakandarasi wa ujenzi wa mradi wa hosteli za wanafunzi unaoendelea katika Chuo Kikuu Mzumbe wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya ujenzi huo.
Mradi huo unaogharimu Shilingi bilioni 6.5 unahusisha ujenzi wa Majengo manne ya ghorofa ya hosteli za wanafunzi ambayo yatachukua wanafunzi 1,024 kwa mara moja pindi yatakapokamilika. Mradi huo pia unahusisha ujenzi wa nyumba za waangalizi pamoja na maeneo ya kufulia na kuanikia nguo za wanafunzi.
Aidha,Waziri Ndalichako ametoa pongezi kwa SUMA JKT kwa kutekeleza mradi huo kwa kasi na kwa ubora huku akiwataka wakandarasi wengine wanaofanya kazi katika miradi mbalimbali ya ujenzi ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kuiga mfano wa SUMA JKT katika utendaji.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akikaga baadhi ya majengo ya hosteli za wanafunzi yanayoendelea kujengwa katika Chuo Kikuu Mzumbe. Mradi huo unafadhiliwa na serikali. 
Nae Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. Lughano Kusiluka ameishukuru Serikali ya Awamu ya Tano kwa uwekezaji mkubwa uliofanyika katika kuboresha miundo mbinu ya Chuo hicho katika Kampasi ya Mbeya na Kampasi Kuu Morogoro, akieleza kuwa uwekezaji wa kiasi hicho kwa Chuo Kikuu Mzumbe haujafanyika kwa zaidi ya miaka 40.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akikapata maelezo juu yamradi wa ujenzi wa hoasteli za wanafunzi katika Chuo Kikuu Mzumbe .

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni