Jumapili, 12 Januari 2020

HAFLA YA UWEKAJI JIWE LA MSINGI SKULI YA MWANAKWEREKWE ZANZIBAR

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli Januari 11, 2020 ameweka jiwe la Msingi katika Skuli Mwanakwerekwe, Zanzibar.
 
Hafla hiyo ya uwekaji wa jiwe la msingi imehudhuriwa na Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako pamoja na Viongozi mbalimbali wa Serikali.
Akihutubia wananchi waliohudhuria katika hafla hiyo Rais  John Pombe Magufuli ameipongeza Serikali ya Awamu ya Saba kwa miaka tisa kwa kuiletea Maendeleo Zanzibar ikiwemo Sekta ya Elimu, huku akiwataka Viongozi katika Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kusimamia katika kuongeza ufaulu wa Shule za visiwani katika mitihani ya kitaifa.
Amesema katika kipindi cha miaka tisa idadi ya wanafunzi imeongezeka katika skuli za Maandalizi kutoka 238 mwaka 2010  na kufikia wanafunzi 382 kwa mwaka 2018. Kwa upande wa Sekondari idadi imefikia wanafunzi 381 kutoka 299 mwaka 2010 na Vyuo Vikuu  kutoka 767 mwaka 2010 na kufikia Wanafunzi 3,624 mwaka 2018.
 
Skuli ya Mwanakwerekwe inajengwa kwa  gharama ya shilingi Bilioni 2.628 ambazo ni  mkopo wa Dola milioni 35 ambazo ni zaidi Bilioni 80 kutoka Benki ya Dunia na  zimejenga skuli mbalimbali ikiwemo Mwanakwerekwe.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni