Jumanne, 23 Septemba 2014

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
MINISTRY OF EDUCATION AND VOCATIONAL TRAINING

COMMONWEALTH SCHOLARSHIPS TENABLE IN THE UNITED KINGDOM FOR THE YEAR 2015
The Ministry of Education and Vocational Training as a nominating agent in the country for the Commonwealth scholarships in inviting applications from qualified Tanzanians for Masters and Doctorate degrees tenable in the United Kingdom in the year 2015.

The Scholarships include:
·         One year taught masters courses of equivalent degrees.
·         Doctorate degrees of up to three years duration.

Qualifications
1.      Applicants must be holders of bachelor of masters degrees;
2.      Applicants for masters must have bachelor degrees of GP A not less than 3.5; and
3.      Applicants for Doctorate degrees must have a B Grade Masters degrees or a GPA 4.0 or above at Masters level.

Mode of Application:
·         All applications should be made directly to the Commonwealth Secretariat and should be online using the following link:http://bit.ly/cscuk-apply.

·         It is important that applicants should read and understand all given instructions when filling the application forms, and should attach all necessary attachmentssuch as certified copies of academic certificates, transcripts, birth certificates and submit online through the above mentioned link.

All applicants who wish to be nominated by the Ministry of Education and Vocational Training, should print one hard copy of completely filled application form, attach with certified photocopies of academic certificates, transcripts and birth certificates and submit them to the address below before 31st October, 2014.

The Permanent Secretary,
Ministry of Education and Vocational Training,
P.O. Box 9121,

DAR ES SALAAM.

Alhamisi, 11 Septemba 2014

WAZIRI KAWAMBWA AWAAGIZA WAMILIKI WA SHULE KUFANYIA KAZI RIPOTI ZA UKAGUZI.



Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dkt. Shukuru Kawambwa amewataka Wakaguzi wa Shule kuhakikisha ripoti wanazotoa kwa wamiliki wa shule, shule, bodi za shule na kwa walimu baada ya ukaguzi shuleni  zinafanyiwa kazi mara moja ili kupunguza changamoto zinazoikabili sekta ya Elimu. 

Mhe. Dkt Kawambwa aliyasema hayo hivi karibuni jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya Ukaguzi kitaifa iliyofanyika katika ukumbi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Dar es salaam (DUCE).
 “Wamiliki wa shule mnapaswa kufanyia kazi ripoti zinazotolewa na Wakaguzi wa Shule badala ya kuziweka katika makabati,  lazima tuhakikishe  mapungufu yote yaliyobainishwa yanapatiwa ufumbuzi mara moja ili kuninua ubora wa Elimu.”  Alisema Dkt. Kawambwa.

Aidha, amesema ni aibu kwa Wakaguzi wa Shule kuendelea kukagua na kukutana na changamoto zilezile ambazo walikutana nazo wakati walipofanya ukaguzi kwa mara ya kwanza na kuzitolea ripoti kwa wamiliki wa shule na bado hazifanyiwi kazi..

Hata hivyo Dkt. Kawambwa, aliwambia  wadau wa Elimu kuwa zipo changamoto nyingi zinazoikabili sekta ya Elimu, ambazo ni pamoja na uhaba wa rasilimali watu, rasilimali fedha, utendaji na usimamizi mbovu, msongamano wa wanafunzi darasani, utoro, uhaba wa walimu wa masomo ya sayansi na hisabati, uhaba wa Majengo,  na uhaba wa maabara.

Waziri amesema changamoto nyingi katika sekta ya Elimu zinatokana na ukosefu wa ushirikiano kati ya Wizara na wadau wa Elimu, na hivyo basi kuwaomba wazazi na jamii kwa ujumla kushirikiana kwa pamoja ili kuleta  mabadiliko makubwa katika sekta ya Elimu.

Dkt. Kawambwa amewataka wananchi na wadau wa Elimu kuwauliza wakaguzi wa shule, ni mara ngapi wamezikagua shule na wameshauri nini na je ushauri huo umezingatiwa na kufanyiwa kazi, yote hayo yanahitajika ili kufanikisha Mpango mpya wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now-BRN).

Waziri akiitimisha hotuba yake katika kongamano hilo la wiki ya ukaguzi aliwasihi wadau wa Elimu kuitumia vizuri kauli mbiu ya maadhimisho hayo inayosema “Ukaguzi Fanisi Na Endelevu Kwa Elimu Bora” kujadili kwa kina  mada zote  katika kongamano hilo zitakazo wasilishwa na wataalamu ili kupata matokeo yanayotarajiwa katika sekta ya Elimu nchini.












WAZAZI WATAKIWA KUSIMAMIA NIDHAMU YA WATOTO



Waziri wa Elimu na Mafunzo  ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Kawambwa  amewataka  wazazi kusimamia ipasavyo maadili ya watoto wao ili waweze kufanikiwa na kufikia malengo  waliyojiwekea kitaaluma. Pia aliwataka kushirikiana na walimu katika kuhakikisha watoto wanakuwa na nidhamu ya kuridhirisha katika jamii inayowazunguka.   

Dkt Kawambwa alitoa wito huo katika mahafari ya kuwatunuku vyeti wanafunzi wa darasa la saba katika shule ya Msingi  Kongo iliyopo Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani. Ambapo aliwataka walimu na wazazi kuhakikisha wanawasisitiza wanafunzi kutii sheria za shule kama vile uvaaji wa sare sahihi ya shule, kuheshimiana na utumiaji wa lugha nzuri.

“Wazazi tuna jukumu kubwa la kusimamia suala la maadili ya  watoto wetu. Hili ni suala ambalo huwezi kulitenanisha na mafanikio bora kitaaluma. Mara nyingi mtoto wenye nidhamu na maadili mema daima hufanya vizuri darasani na yule asiye na nidhamu huporomoka katika taaluma. Nasisitiza nidhamu na taaluma huenda pamoja, haiwezekani kuvitenganisha hata mara moja.” Alisisitizi Dkt. Kawambwa.
Aidha, aliwataka wanafunzi wote nchini wanaomaliza darasa la saba kujiandaa vyema kufanya Mitihani yao inayotarajiwa kuanza,  kujitahidi kutulia na kutumia vyema maarifa yote waliyopata kutoka kwa walimu wao. Aliwakumbusha kwamba watakapomaliza mitihani yao wasijisahau na kufikiri kuwa sasa elimu ndio basi bali watambue kuwa safari ya kutafuta elimu ndio inaanza.

Dkt Kawambwa aliwataka kutenga muda wa kujiandaa kwa masomo ya sekondari mara wanapomaliza mitihani yao ya darasa la saba. "Nawasihi muwe raia wema wenye kuwajibika katika jamii yote. Maisha sio lele mama! wekeni juhudi katika masomo, elimu ndio msingi bora wa maisha, msidanganyike hakuna njia ya mkato katika kufanikiwa katika maisha".  aliongeza Dkt. Kawambwa. 
Waziri Kawambwa aliwataka walimu wote nchini kutambua kuwa shughuli za kila siku shuleni zinahitaji juhudi za hali ya juu. Aliwataka kuboresha  zaidi utendaji kazi wao ili kufikia matarajio ya Taifa ya kuwa na  watu walioelimika na wenye uwezo wa kuhimili  changamoto zinazotokana na mabadiliko ya Sayansi na Teknolojia.

Waziri aliwasisitiza walimu kukabiliana na changamoto zinzojitokeza katika sekta ya elimu kwa kuacha kufanya kazi kwa mazoea, badala yake kuhakikisha wanapanga mipango yao, wanajiwekea malengo ya muda mfupi na mrefu na kubuni mikakati sahihi inayotekelezeka ambayo itawezesha kufikia malengo waliyojiwekea.  

Aidha, aliwashauri wazazi  kutoa ushirikiano wa hali ya juu katika suala zima la kufanikisha matokeo mazuri ya ufaulu kuanzia madarasa ya awali, la kwanza hadi darasa la Saba. "Yote haya yanawezekana pale tutakapotekeleza wajibu wetu wa kusimamia vyema yale yote wanayofundishwa watoto wetu wanapokuwa shuleni. Watoto hupewa mazoezi mbalimbali (homework) na walimu wao ili wazifanye wanapokuwa nyumbani, ni jambo la msingi tukitenga muda kusimamia katika eneo hili. "

  Pia aliwataka wazazi kuhakikisha wanatimiza jukumu lao la kuwapatia watoto mahitaji muhimu yanayotakiwa shuleni.  Kwani mara nyingi utoro wa Wanafunzi shuleni huchangiwa sana wanafunzi wanapo shindwa kupatiwa mahitaji yao ya shule.

Aliwataka wanafunzi wanaobaki shuleni kujitahadi  kuzingatia Masomo. Kwani kipindi walichonacho shuleni ni kifupi sana, lakini ni kipindi  muhimu sana katika kuandaa maisha yao ya baadaye. Amewataka kuwasikivu, kutii sheria za shule, tekeleza majukumu yao wanayopewa katika masomo, kuepuka vitendo viovu katika jamii. Alwasihi kuwa na nidhamu inayopendeza machoni na mioyoni mwa wazazi, walezi na walimu wao. 

Shule ya Msingi Kongo ilianzishwa mwaka 1976 ikiwa na wanafunzi 38 na sasa ina wanafunzi 612 kuanzia Darasa la Awali hadi Darasa la Saba. Wanafunzi 72 wanaohitimu Elimu ya Msingi katika Shule hii mwaka huu.. 

















Jumanne, 2 Septemba 2014

NAIBU WAZIRI AWAAGIZA MAAFISA ELIMU KUWARUDISHA WANAFUNZI WATORO SHULENI


Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe.Jenista Mhagama amewaagiza Maafisa Elimu wote nchini kuhakikisha wanafunzi walioacha shule kwa sababu mbalimbali wanarudi shuleni ili kuendelea na masomo.

Naibu Waziri alitoa agizo hilo mwishoni mwa wiki  wakati wa ziara yake mkoani Pwani kukagua miradi inayojengwa na Mpango wa Maendeleo  ya Elimu ya Msingi (MMEM) na Mpango wa Elimu ya Sekondari (MMES). Shule zilizotembelewa ni Nyamisati, Mkamba na WAMA Nakayama zote zikiwa za sekondari na shule ya Msingi ya Mazoezi Vikindu, .

Aliwataka Maafisa Elimu  kufuatilia  sababu za utoro unaojitokeza shuleni na kuandika taarifa juu ya utoro huo na kutafuta njia za kupunguza utoro shuleni. Pia aliwataka Wakaguzi wa Shule wa Kanda pamoja na kazi nzuri wanayoifanya ya kukagua ufundishaji na vigezo, ukaguzi unaofanyika sasa ujikite  katika kujibu hoja ya utoro wa wanafunzi katika shule. Alimuagiza Kaimu Mkurugenzi wa Ukaguzi wa Shule kutoka Wizarani Bibi Hidaya Mohamed kutopokea ripoti zisizotoa uelekeo wa namna ya kuwarudisha watoto shuleni.
“Katika kila shule ambapo kutakuwa na utoro mkubwa wa wanafunzi Wakaguzi msipokee ripoti ya ukaguzi isiyotoa majibu kwanini wanafunzi katika shule zetu za msingi na sekondari wanaendelea kutoroka na ripoti ionyeshe hatua zilizochukuliwa kuwarudisha shuleni, mipango na mikakati ya kuhakikisha suala hili halijirudii ili kuwa na ubora wa elimu.” Alisema Mhe. Mhagama   

 Kuhusiana na maslahi ya Walimu Mhe. Mhagama alimtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mkuranga kuanzisha dawati la malalamiko litakalowawezesha walimu  kupeleka malalamiko yao  na kuwataka yafanyiwe kazi haraka iwezekanavyo. Alisema kuanzishwa kwa dawati hilo kutawapunguzia adha walimu ya kupoteza muda kufuatilia madai yao na badala yake watatumia muda huo kuwafundisha wanafunzi.
                                      
“Sitaki walimu hawa tunaowaleta huku wapoteze muda mwingi katika majengo ya Halmashauri kufuatilia madai yao kwani hawa ndio watumishi wengi kwenye Halmashauri hakikisheni mnawatengea dawati maalumu la kushughulikia kero zao.”Alisema Mhe.  Mhagama.






Waraka wa elimu na. 4 wa mwaka 2014 kuhusu utayarishaji wa vifaa vya kujifunzia na kufundishia

Jumatatu, 25 Agosti 2014

Waziri Kawambwa aiasa Jamii Kuchangia Elimu

 Aipongeza Airtel kwa kutoa vitabu

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dkt. Shukuru Kawambwa ameiasa jamii kuchangia kuboresha elimu nchini kwa kutoa misaada mbalimbali itakayosaidia kuimarisha ubora wa elimu inayotolewa katika ngazi mbalimbali za elimu.

Waziri Kawambwa alikuwa akizungumza katika hafla  ya uzinduzi wa Mradi wa Vitabu Airtel Shule Yetu 2014 jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki ambapo wawakilishi wa shule  za Sekondari 30 walipatiwa msaada wa vitabu vya Sayansi na Hisabati na Kampuni hiyo.




Waziri Kawambwa ambaye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo alisema Mradi huu wa Vitabu Airtel Shule Yetu utakuwa wa manufaa makubwa sana si kwa  wanafunzi shuleni tu bali kwa sekta nzima ya Elimu hapa nchini na kwa Taifa kwa ujumla.  

Sote tunatambua kwamba kitu pekee kinachotofautisha nchi zilizoendelea na zinazoendelea siyo utajiri na mali walizonazo bali ni elimu na ujuzi.  Hii ni kwa sababu utajiri na mali havijileti vyenyewe isipokuwa huchochewa na maendeleo mazuri yaliyo jengwa katika msingi mzuri wa ELIMU. Kwa kadri kiwango cha elimu na ujuzi au maarifa kinapokuwa juu katika nchi, ndipo na kiwango cha maendeleo ya nchi yanapozidi kukua katika nchi hiyo,”alisema Dkt. Kawambwa.

Dhamira ya Dira ya Maendeleo ya Mwaka 2025 (Tanzania Development Vision 2025) ni kuifanya Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.  Lakini hilo litawezekana tu kwa kupitia elimu.  Yaani kuwa na Taifa lililoelimika; lenye wasomi wanaoweza kubaini na kutatua matatizo ya maendeleo ya nchi yetu.  Na katika wakati huu tulionao, Sayansi na  Tekinolojia vina nafasi  ya  pekee katika maendeleo ya nchi na ustawi wa jamii. 

“Tunaishukuru sana Airtel Tanzania kwa kutuunga mkono katika dhamira ya Serikali yetu ya kuwekeza katika sekta ya elimu nchini.  Airtel imekuwa mstari wa mbele katika kuchangia vitabu pamoja na misaada mbalimbali kwa shule zetu hapa nchini.  Vitabu hivi vilivyochangiwa na Airtel vitasaidia sana katika juhudi za Serikali za kuimarisha ubora wa elimu inayotolewa,” alisema Waziri Kawambwa. 


Hivi sasa kuna uhaba wa walimu wa masomo ya Sayansi na Hisabati katika shule zetu za Sekondari hapa nchini.  Takwimu zinaonesha kwamba hadi mwaka 2013/14 tulikuwa na upungufu wa walimu wa Sayansi na Hisabati 26,998.  Lakini hata kule kwenye walimu wa masomo haya bado kuna tatizo la uhaba wa vitabu.  Lakini kule ambako kuna uhaba wa walimu uwepo wa vitabu hivi utakuwa ni wa msaada sana kwa wanafunzi kuweza hata kujisomea wenyewe.  

Tukio hilo la Kampuni ya Airtel kukabidhi vitabu ni mwendelezo wa mambo mengi ambayo yamekwishafanya katika kuisadia Sekta ya elimu nchini.  Mradi huu ulianza miaka takriban kumi iliyopita na katika kipindi chote hiki mradi umeweza kupeleka vitabu na vifaa vya maabara katika shule mbalimbali na pia kufanya ujenzi na matengenezo katika shule kadhaa hapa nchini.  

Napenda kutumia fursa hii kuwahimiza makampuni mengine  na Taasisi mbalimbali nchini kuiga mfano huu wa Airtel na kusaidia sekta ya elimu ili kujenga taifa lililo bora.  Serikali iko tayari kushirikiana na Taasisi, Makampuni na asasi mbalimbali katika kuendeleza Elimu ya watoto na vijana wetu,” alisema Waziri Kawambwa. 

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa Airtel Tanzania Sunil Colaso alisema kampuni yake itaendelea kuisaidia sekta ya elimu ili kuchangia katika juhudi za serikali za kuboresha elimu hapa nchini ambapo hadi hivi sasa shule za sekondari 1,000 zimefaidika kwa kupewa vitabu na kampuni hiyo.