Jumatatu, 19 Februari 2018

TAARIFA KWA UMMA



TAARIFA KWA UMMA
Nimepokea kwa masikitiko makubwa sana taarifa ya kifo cha Akwilina  Bafhata Akwiline aliyekuwa mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika Chuo cha Usafirishaji (NIT).
Kifo hicho kimetokea wakati askari wakiwa wanadhibiti maandamano yaliyokuwa yakifanyika tarehe 16/02/2018 kwenye eneo la Mkwajuni Wilaya ya kinondoni, jijijini Dar es salaam.

Napenda kutumia fursa hii kutoa pole sana kwa Familia ya Ndugu,  jamaa na marafiki wote wa Akwilini.  Pia napenda kutoa pole kwa Uongozi na Jumuia ya Chuo cha Usafirishaji, wanafunzi wote nchini na wananchi wote kwa ujumla.

Ndugu Akwilini ni binti aliyekuwa anatambua na kuthamini umuhimu wa Elimu, na alijitoa kuhakikisha kuwa anasoma kwa bidii kwa manufaa yake binafsi, familia yake na kwa manufaa mapana ya taifa taifa.  Kifo chake kimetokea wakati akiwa kwenye kutekeleza wajibu wake kama mwanafunzi wa kupeleka barua mahali alipokuwa anatarajia kufanya mazoezi kwa vitendo yatakayoanza tarehe 27/02/2018. Kifo hicho cha kusikitisha kimezima ndoto yake Serikali ikekipokea kwa masikitiko makubwa sana. 

Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Joseph Pombe Magufuli amesikitishwa  na kuhuzunishwa sana na kifo cha mwanafunzi Akwilini na anaungana na familia, ndugu jamaa na watanzania wote kuwapa pole za dhati kutokana na msiba huo. 
Serikali inatumia fedha nyingi kuwasomesha wanafunzi kuanzia Elimu msingi, sekondari na hutoa mikopo kwa wanafunzi wa Elimu ya juu kwa sababu tunatambua mchango wa Elimu katika maendeleo ya nchi yetu. Marehemu Akwilini alikuwa ni miongoni mwa wanufaika wa Mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu. 

Mimi  Waziri mwenye dhamana ya  sekta ya Elimu nimesikitika sana kuona binti huyo amepoteza maisha yake akiwa katika kutekeleza shughuli za kielimu.

Wizara yangu itagharamia shughuli zote za mazishi ya Marehemu Akwilina hadi hapo atakapopumzishwa katika makao yake ya milele. 
Namuagiza Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Dk. Leonard Akwilapo kusimamia shughuli zote za msiba huo hadi  Akwilina atakapozikwa katika nyumba yake ya milele. 

Nitumie fursa hii kuviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuwafikisha mara moja wahusika waliosababisha kutokea kwa tukio hilo kwenye vyombo vya sheria ili  wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria za nchi yetu.

Nawasihi sana watanzania wenzangu tujiepushe kukiuka tarataibu na miongozo inayokuwa inatolewa ikiwemo  maandamano na vitendo vyote ambavyo vinaweza kusababisha maafa kwa watu wasio na hatia.

Mungu aiweke roho ya Marehemu Akwilini mahala pema peponi Ameni

Imetolewa na:

Prof Joyce Lazaro Ndalichako
Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia.
18 / 02/2018


Katibu MKuu Akwilapo: awataka watumishi wa wizara yake kufanya kazi lea bidii na weledi


Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Leonard Akwilapo amewataka watumishi wa wizara hiyo kufanya kazi kwa bidii na  kuzingatia weledi katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku.

Dk. Akwilapo ameyasema hayo wakati wa kikao cha kwanza cha watumishi wa wizara hiyo kilichofanyika mkoani Dodoma tangu serikali itangaze rasmi kuhamishia makao makuu ya nchi mkoani humo.

Dk. Akwilapo amesema utii, ushirikiano,bidii na upendo mahali pa kazi miongoni mwa watumishi ndiyo silaha pekee ya kufikia malengo ambayo Wizara imejiwekea katika kuinua Sekta ya Elimu hapa nchini.

"Nipende kuwapongeza watumishi wote kwa kushiriki majukumu mbalimbali ya Wizara ikiwemo kuisimamia vyema miradi mbalimbali inayotekelezwa na Wizara, nawasihi sana tuusifanye kazi kwa kujitenga, ushirikiano miongoni mwetu ni jambo la msingi sana na tukiwa na Umoja basi mafanikio lazima yatapatika katika Sekta hii ya Elimu,"alisema Dk.Akwilapo.

Pia Katibu Mkuu Dk.Akwilapo amewataka watumishi kuwa na matumizi sahihi ya Teknolojia,kujibu barua mbalimbali kwa wakati pamoja na kushughulikia faili zinazofika kwenye ofisi zao ndani siku mbili  na siyo kuziacha zikae muda mrefu.


Kupitia kikao hicho watumishi pia walipata fursa ya kuwaaga viongozi ambao walitumikia Wizara hiyo ambao hivi sasa wamehamiahiwa Wizara nyingine na kuwakaribisha viongozi wapya ambao wamehamia kwenye Wizara hiyo.

Viongozi waliokaribishwa ni pamoja na Naibu Waziri William Ole  Nasha na Naibu Katibu Mkuu Profesa  James Mdoe na walioagwa ni Naibu Waziri Mhandisi Stella Manyanya na Profesa Saimon Msanjila ambaye hivi sasa ni Katibu Mkuu anayesimamia Sekta ya Madini.





Alhamisi, 15 Februari 2018

TBA yatakiwa kulipa madeni ya wananchi katika ujenzi shule ya wavulana Ihungo


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako amewataka wakala wa majengo nchini TBA kulipa madeni wanayodaiwa na Wananchi mbalimbali kufuatia ujenzi unaoendelea wa Shule ya Sekondari wavulana Ihungo iliyopo Wilayani bukoba mkoani kagera.

Waziri Ndalichako amesema kuwa tayari wizara imekwisha ilipa TBA  zaidi ya bilioni Tisa na garama ya ujenzi kwa mradi wote ni shilingi  bilioni 10 nukta 48.

" Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni,  nipende kuwapongeza Wakala wa Majengo TBA kwa kazi nzuri ambayo wameifanya.

"Lakini nasikikitika sana kupokea malalamiko kutoka ofisi ya Mkuu wa mkoa inayoeleza kuwa bado kuna Wananchi wanaidai TBA kutokana na kutoa vifaa mbalimbali vya ujenzi kama vile mbao, matofali, na vibarua ambao wameshiriki katika ujenzi huo wa shule ya wavulana Ihungo na kuwa mpaka sasa hawajalipwa, hii haipendezi ni vyema TBA kuhakikisha inalipa madeni hayo,"alisema Waziri Ndalichako.

Waziri Ndalichako amesema haoni sababu kwa nini wananchi hawajalipwa wakati tayari Serikali imekwisha ilipa TBA, ni vyema wakalipwa ili kusaidia kuepusha migogiro isiyo ya lazima baina ya Serikali na wananchi.

Kwa upande wake Meneja wa TBA mkoa wa  Kagera Salum Chanzi amekiri kuwepo kwa sababu mbalimbali zilipelekea mradi kutokamilika kwa wakati na hivyo kuomba wapewe muda zaidi mpaka mwezi machi mwaka huu ili waweze kukamilisha.

"Mheshimiwa Waziri mradi huu haijakamilika kwa wakati uliokuwa umepangwa kutokana na changamoto ya kuagiza vifaa kutoka nje ya mji wa bukoba, na hii inatokana na bei wakati mwingine kuwa kubwa hapa bukoka  lakini nje ya hapa tunavipata kwa bro nafuu," alisema Chanzi.

Chanzi amemhakikishia Waziri Ndalichako kuwa tayari madeni yote wanayodaiwa na wananchi katika ujenzi huo wa Ihungo Sekondari yamewasilishwa kwenye Taasisi yake yanafanyiwa kazi na wahusika wote  watalipwa.






CHINESE GOVERNMENT SCHOLARSHIP APPLICATION FOR 2018/2019

The general public is hereby informed that the 2018/2019 Chinese Government Scholarship is now open for application.  Online application and corresponding application documents should be submitted to application receiving agency not later than April 1st, 2018.  For more information, please refer to http://www.csc.edu.cn/studyinchina or www.campuschina.org

Eligibility:
To be eligible, applicants must
·        Be citizen of a country other than the People’s Republic of China, and be in good health;
·        Be a high school graduate under the age of 25 when applying for master’s programs;
·        Be a bachelor’s degree holder under the age of 35 when applying for master’s programs;
·        Be a master’s degree holder under the age of 40 when applying for doctoral programs;
·        Be under the age of 45 and have completed at least two years of undergraduate study when applying for general scholar programs;
·        Be a master’s degree holder or an associate professor (or above) under the age of 50 when applying for senior scholar programs.
Application Documents
a)     Application Form for Chinese Government Scholarship (in Chinese or English);

b)     Certified highest diploma: Prospective diploma winners must submit official proof of student status by their current school.  Documents in languages other than Chinese or English must be attached with certified Chinese or English translations;

c)      Academic transcripts:  Transcripts in languages other than Chinese or English must be attached with certified Chinese or English translations;

d)    A Study Plan or Research Proposal in Chinese or English.  (A minimum of 200 words for undergraduates, 500 words for non-degree students, and 800 words for postgraduates);

e)     Recommendation letters:  Applicants for graduate programs or senior scholar programs must submit two letters of recommendation in Chinese or English from professors or associate professors;

f)      Applicants for music studies are requested to submit their own works.  Applicants for fine arts programs must submit their own works which include two sketches, two color paintings and two other works;

g)     Applicants under the age of 18 should submit the valid documents of their legal guardians in China; and

h)    Applicants planning to stay in China for more than 6 months must submit a photocopy of the Foreigner Physical Examination Form completed in English (the original copy should be kept by the applicant.  The form designed by the Chinese quarantine authority can be downloaded from http://www.csc.edu.cn/studyiinchina or www.campuschina.org.  The physical examinations must cover all the items listed in the Foreigner Physical Examination Form.  Incomplete records or those without the signature of the attending physician, the official stamp of the hospital or a scaled photograph of the applicants are invalid.  Please select the appropriate time to take physical examination as the result is valid for only 6 months.

Please submit the following documents where applicable
i)       Pre-admission Letter from Chinese Government Scholarship universities; and

ii)       Language qualification certificate. E.g., HSK certificates, IELTS or TOFEL report.


ONLINE APPLICATION OF THE CHINESE GOVERNMENT SCHOLARSHIP INFORMATION SYSTEM

Step 1:  Visit http://www.csc.edu.cn/laihua or www.capuschina.org and click “Scholarship Application Online for International Students”.
Step 2:   Read “Tips for online application”      carefully before clicking “NEXT” to the registration page.
Step 3:   Log in with your user name and password.  For new user, please click “Create an account” for registration.
Step 4:   Fill in the correct Program Category and Agency Number.  An Agency Number represents a specific application receiving agency and a correct choice of Program Category is necessary before filling in the Agency Number.  Please make sure you fill it in correctly, otherwise you will not be able to continue your online application or your application will not be accepted.
Your ‘Program Category’ is:  Type A and Agency Number is:  8341.  Once the correct ‘Agency Number’ is entered, the name of the agency will automatically emerge.
Step 5:   Fill in the Online Application Form and Upload Supporting Documents truly, correctly and completely following the steps listed on the left of the page.
Applicants are required to select a discipline before choosing their majors.  Please refer to the Disciplines Index, which could be downloaded from help, if you have any doubt about the disciplines and majors.
Step 6:   Check each part of your Application carefully before submitting it.  Click Submit to submit your Application.  The submitted documents will be the only reference for the applied universities to confirm the admission.
Step 7:   You can make changes to your application by clicking Withdraw and Edit the Application on the top of the page.  But make sure to submit it again by clicking Submit after finishing all the changes.  Otherwise, the retrieved application will become invalid and your new application will not be received either.
Step 8:   You can download and print the completed Application Form by clicking Print the Application Form.
Step 9:   Send the paper application form and other supporting documents to the dispatching authorities if they require you to do so.
Please note that only Chinese and English are accepted for the online application.

Kindly submit your application to the undersigned not later than 1st April, 2018
Executive Secretary,
Tanzania Commission for Universities,
Mlimani Tower, Sam Nujoma Road,Opposite Mliman City,
P. o Box 6562, Dar es Salaam-Tanzania.


Waziri Ndalichako :Maafisa Elimu Nchini fuateni Sera na Miongozo inayotolewa na Wizara


Maafisa Elimu nchini wametakiwa kufuata miongozo na sera inayotolewa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia wakati wa kutekeleza majukumu yao na endapo watakiuka maelekezo hayo wahusika watachukuliwa hatua za kisheria.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akiwa Wilayani Muleba mkoani Kagera na kusema kuwa kumekuwa na tabia kwa baadhi ya  Maafisa Elimu kupeleka wanafunzi wengi kwenye shule kuliko uwezo wa shule.

Waziri Ndalichako amesema kuwa hali hiyo inachangia kuwepo kwa matokeo mabaya  na hivyo amewaagiza wathibiti ubora wa shule nchini kukagua shule zote ili kuondoa changamoto hizo.

Katika ziara hiyo Waziri Ndalichako pia ametembelea na kukagua shule ya Sekondari ya Profesa Joyce Ndalichako iliyoko Wilayani Muleba ambapo amewaagiza walimu wa shule hiyo kuhakikisha wanafunzi wa shule hiyo wanafanya vizuri kitaaluma.

" Walimu hii shule imebeba jina langu, nawaomba sana matokeo ya shule hii yaendane na Mimi mwenyewe kwa maana ya wanafunzi kufanya vizuri na Wizara itahakikisha inazipatia ufumbuzi changamoto mbalimbali zilizopo katika shule hii," alisema Waziri Ndalichako.

Katika ziara hiyo Waziri Ndalichako alitembelea na kukagua Chuo cha Ualimu katoke, shule ya Sekondari Anna Tibaijuka zilizopo Wilayani Muleba.






Jumatatu, 12 Februari 2018

Katibu Mkuu Akwilapo asisitiza matumizi ya force akaunti kwa FDCs


Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Dk. Leonard Akwilapo leo amefungua mafunzo yanayoelekeza matumizi ya Force Akaunti kwa Wakuu wa Vyuo vya  Maendeleo ya Jamii- FDCs mkoani Morogoro na kusisitiza kuwa utaratibu huo umekuwa na thamani ya matumizi ya fedha, (value for money).
Akizungumza na Wakuu wa Vyuo, Wakufunzi, Maafisa Ugavi na Wahasibu kutoka Vyuo hivyo Katibu Mkuu Akwilapo amesema lengo ni kuwajengea uelewa wa namna ya kusimamia ukarabati ili kuhakikisha Vyuo na Wizara kwa pamoja vinapata thamani ya matumizi ya fedha.

Dk. Akwilapo ameeleza kuwa Force Akaunti  ni utaratibu wa manunuzi ya huduma unaotambulika Serikalini na umekuwa ukitumia sehemu kubwa ya bajeti yake katika ununuzi wa vifaa mbalimbali inayotumika katika ujenzi.

Dk. Akwilapo amesema  lengo la kutumia utaratibu huo ni kupunguza gharama za ujenzi na ukarabati pamoja na kufanya utekelezaji wa mradi kukamilika kwa wakati, kukabiliana na  dharura zinazohitaji kuchukuliwa hatua za haraka pamoja na kuiwezesha taasisi husika kufanya kazi ya ujenzi na ukarabati kwenye taasisi yake pale ambapo ujenzi ni shughuli za kila siku katika Taasisi hiyo.

Ameongeza kuwa Wizara ilitumia wataalam wake katika ujenzi na ukarabati ambapo fedha iliyotumika kwa ajili ya kazi zilionekana kuwa kidogo.

 "Kwa majaribio force Akaunti ilitumika katika halmashauri 129 kujenga madarasa, mabweni, mabwalo, maabaara, Ofisi za walimu, nyumba za walimu  na umeonesha mafanikio makubwa  mahali ambapo kwa kutumia mkandarasi wastani wa shilingi bilioni 2 hadi 3 zingetumika ila kwa utaratibu wa Force Account Wizara imeweza kutumia shilingi milioni 800 hadi bilioni 1 tu".alisema Dk.Akwilapo.

Kwa upande wake mratibu wa mradi wa ESPJ Dk. Jonathan Mbwambo amewataka Washiriki wa mafunzo hayo kuzingatia mafunzo na pia kutumia fedha watakazopewa za ujenzi na ukarabati kama zilivyokusudiwa.

Kati ya vyuo 55 vya FDCs vyuo 20 vitakarabatiwa na kujengwa katika awamu hii ya kwanza ambapo upembuzi yakinifu unatarajiwa kuanza mapema wiki ijayo.
Mafunzo hayo yameratibiwa na mradi wa kukuza stadi za kazi na ajira, ESPJ.





Jumamosi, 10 Februari 2018

Serikali yaridhishwa na ujenzi wa Maktaba ya kisasa UDSM.


Serikali ya Tanzania imeridhishwa na hatua ya ujenzi wa Maktaba ya kisasa pamoja na kuishukuru Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kwa  kujenga Maktaba ya kisasa katika Chuo kikuu cha Dar es salaam ambayo itakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi zaidi ya 2000 na kihifadhi vitabu 800,000 kwa mara moja

Akizungumza mara baada ya kutembelea na kukagua hatua za ujenzi unavyoendelea Chuoni hapo jijini Dar es Salaam Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako amesema Serikali ya China inatambua vipaumbele vya Serikali ya awamu ya Tano hivyo wameahidi kuisaidia Tanzania ikiwa ni pamoja na kuhakikisha vipaumbele vilivyowekwa ikiwemo  Elimu inatimiza malengo yaliyokusudiwa.

Waziri Ndalichako amesema Maktaba hiyo ya kisasa na kubwa barani Afrika pia inajumuisha jengo la Taasisi ya Confucius ambayo imekuwa ikifundisha lugha na tamaduni za kichina kwa wanafunzi wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam  na watanzania, jengo hilo pia linakumbi za Mubashara, pia vyumba vyenye kompyuta za kisasa zenye programu maalumu kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu.

Kwa upande wake Balozi wa Jamhuri ya China hapa nchini Wang Ke amemhakikishia Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako kuwa nchi yake itaendelea kuisaidia Tanzani katika maeneo mbali ikiwemo Sekta ya Elimu.

Ujenzi wa Maktaba hiyo unaotarajiwa kukamilika Julai 2018 utagharimu  dola za kimarekani 41,280, 000.