Ijumaa, 2 Machi 2018

Naibu Waziri Ole Nasha: Kuna ubadhirifu wa fedha za Serikali.


Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.william Ole Nasha ameitaka  ofisi ya Mkuu wa wilaya, Musoma, Polisi na Takukuru kuhakikisha ndani ya wiki mbili inafanya  uchunguzi wa namna fedha za  ujenzi wa Miundombinu ya  Shule ya Sekondari Kasoma zilivyotumika kwa kuwa kuna harufu ya ubadhirifu wa fedha hizo.

Naibu Waziri Ole Nasha ametoa agizo hilo  mkoani Mara baada ya kufanya ziara ya kukagua ujenzi na ukarabati wa Miundombinu ya Shule inayonengwa na Wizara hiyo kupitia programu ya Lipa kulingana na matokeo, (P4R).

Mheshimiwa Ole Nasha amekiri kuridhishwa na ujenzi uliofanyika katika baadhi ya shule za mkoa ambazo amezitembelea ni  pamoja na Shule ya Msingi Kamuguruki  na Shule Sekondari na  Nyasho.

Waziri Ole Nasha pia amewataka walimu  wote nchini kuhakikisha wanafuata maadili yao ya kazi pamoja na kuacha mara moja  kujihusisha na vitendo vya kimapenzi na wanafunzi.

Amesema kuwa wizara yake imepokea taarifa juu ya baadhi ya walimu kujihusisha kimapenzi na wanafunzi  jambo ambalo ni kinyume cha sheria za nchi pamoja na maadili ya utumishi wa umma.

Naibu Waziri huyo amesisitiza kuwa  serikali haitamvumilia mwalimu yeyote mwenye tabia kama hizo na kuongeza kuwa mwalimu atakayebainika kushiriki vitendo hivyo atashtakiwa kwa mujibu wa sheria za nchi.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri  Ole Nasha ameahidi kutoa mabati Mia Tano kwa ajili ya  shule ya sekondari kiara na kujenga madarasa matatu katika shule  Msingi ya Kiara zilizoezuliwa kufuatia mvua kali iliyonyesha jana usiku na kufanya uharibifu wa madarasa mawili ya shule hiyo.

Pia Naibu Waziri Ole Nasha ametembelea chuo cha Maendeleo ya Wananchi Bweri
Kilichopo Wilayani Musoma mkoani Mara.

 Naibu Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Mhe. William Ole Nasha akipata maelezo kutoka kwa wanafunzi wanaosomea  fani ya ufundi umeme kutoka kwenye Chuo cha  Maendeleo ya Wananchi Bweri kilichopo Mkoani Mara.

Naibu Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Mhe.William  Ole Nasha akipata maelezo juu ya hatua za ujenzi wa shule ya Sekondari Kasoma ambapo Naibu Waziro ametoa Wiki mbili kwa Wilaya ya Musoma, Takukuru na Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi mara baada ya kubaini kuwepo kwa ubadhirifu wa fedha za ujenzi katika shule hiyo.

Wakufunzi watakiwa kuzingatia uadilifu na kuweka mbele maslahi ya Taifa.


Naibu Katibu Mkuu Dk.Ave Maria Semakafu amewataka Wakufunzi nchini kuwa waadilifu na kutanguliza maslahi ya Taifa mbele siku zote wanapotekeleza majukumu yao ya kazi.

Dk.Semakafu ametoa rai hiyo mkoani Mwanza wakati akifungua mafunzo ya TEHAMA kwa wakufunzi wa Vyuo vya Ualimu yaliyofanyika katika Chuo cha Ualimu Butimba mkoani humo.

Naibu Katibu Mkuu huyo amesema lengo la mafunzo ni kuwa na maudhui yenye viwango vya ubora unaotakiwa ili kuleta ufanisi katika kujifunza na kufundisha hususan katika  kuandaa Walimu. 

Dk. Semakafu amesisitiza kuwa  mafunzo hayo yatawajengea umahiri na hatimaye kuwa na rasilimali watu yenye maarifa na umahiri kwa ajili ya uzalishaji na hatimaye kukuza uchumi na kufikia malengo ya nchi kwa kuwa na uchumi wa kati na Uchumi wa Viwanda ifikapo 2025. 

" Zipo  changamoto katika Sekta  ya Elimu, sasa lazima tuzitafutie ufumbuzi wa  namna ya kuzikabili kwa kutumia mfumo wa kidigitali ili kuboresha ufundishaji na pia kubadilishana taarifa na maarifa," amesema Dk. Semakafu.

Kwa upande wake mratibu wa Mradi huo  Ignas Chonya amesema Mradi wa Teacher Education Support Project (TESP) utawezesha kufanikisha  umahiri wa mwalimu kupitia mafunzo kazini ya wakufunzi katika maeneo mbali mbali ikiwemo mafunzo ya TEHAMA, mafunzo endelevu katika masomo wanayofundisha, mafunzo ya Uongozi wa Elimu,  ambayo ndiyo nguzo muhimu katika kufanikisha upatikanaji wa Elimu bora hapa nchini.

Wakufunzi walioshiriki Mafunzo hayo ya Siku Tisa ni kutoka katika Chuo cha Ualimu Butimba,Tabora, Shinyanga, Ndala,Murutunguru, Bunda, Katoke, Tarime,Kasulu na Kabanga.

Mradi wa TESP unatekelezwa na Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Canada kupitia Idara yake DFATD kwa ajili ya kugharamia mradi huo kwa kuweka kipaumbele cha kuleta mabadiliko chanya katika Elimu ya Ualimu.
 Naibu Katibu Mkuu Dk. Avemaria Semakafu akisalimiana na viongozi mbalimbali baada ya kuwasili katika Chuo cha Ualimu Butimba kilichopo mkoani Mwanza.

 Baadhi ya Wakufunzi kutoka Vyuo 10 vya Ualimu hapa nchini wakishiriki mafunzo ya TEHAMA, yanayoendeshwa na  TESP.

Naibu Katibu Mkuu Dk. Avemaria Semakafu akionyesha rasimu ya kitabu ambacho ndiyo mwongozo katika kujifunzia TEHAMA kwa Wakufunzi.

Jumanne, 27 Februari 2018


INVITATION TO TENDER

UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

MINISTRY OF EDUCATION SCIENCE AND TECHNOLOGY



CONSTRUCTION WORKS FOR MPWAPWA TEACHERS COLLEGE

NATIONAL COMPETITIVE BIDDING (NCB)

SPECIFIC PROCUREMENT NOTICE (SPN):

Loan No. 2100150031995
Project ID No.: P-Z1-IB0-016
Tender No.:  ME-024/2017-18/HQ/W/14
1.         This Invitation for Bids follows the General Procurement Notice (GPN) for this project that appeared in UNDB online with reference number AfDB34-01/15 of 20th January 2015, and on the African Development Bank Group’s Internet Website.
2.         The United Republic of Tanzania has received Financing from the African Development Bank in various currencies towards the cost of Support to Technical Vocational Education and Training and Teachers Education (STVET-TE).  It is intended that part of the proceeds of this loan will be applied to eligible payments under the contract for Construction Works for MPWAPWA Teachers College.
3.         The Permanent Secretary, Ministry of Education, Science and Technology (MoEST) now invites sealed bids from eligible bidders who meet qualifications criteria as stated in Bidding Document and are registered with the Contractors Registration Board of Tanzania as Building Contractor in Class four and above for the construction works for MPWAPWA Teachers College
4.         Interested eligible bidders may obtain further information from and inspect the bidding documents at the office of Secretary, Ministerial Tender Board, Ministry of Education, Science and Technology, College of Business Studies and Law Universities of Dodoma (UDOM) Block 10, Room no.320, 40479 DODOMA, TANZANIA Tell: 026 – 2963533 from 08.00 to 15.00 hours, Mondays to Fridays inclusive, except on public holidays.

5.         A complete set of bidding documents may be purchased by interested bidders on the submission of a written application to the above address and upon payment of a non-refundable fee of TZS. 150,000.00(Tanzania shillings one hundred thousand only)
6.         The provisions in the Instructions to Bidders and in the General Conditions of Contract are the provisions of the African Development Bank Standard Bidding Document:  Procurement of Goods.
7.            Bids must be delivered to the above office on or before 10.30HRS on Tuesday, 27th Mach 2018 and must be accompanied by a bid security in acceptable form (in the form of bank guarantee) of Tanzanian Shillings Twenty Million (20,000,000/=).


8.            Bids will be opened in the presence of bidders’ representatives who choose to attend at 10.45HRS on Tuesday, 27th Mach, 2018 at the offices of Ministry of Education, Science and Technology, College of Business Studies and Law, Universities of Dodoma (UDOM) Block 10, Ground Floor, Conference Room.


Permanent Secretary
Ministry of Education, Science and Technology
UDOM Block 10, P.O. Box 10,
40479DODOMA


Jumatatu, 26 Februari 2018

China na Korea kuisaidia Tanzania katika Sekta ya Afya na Elimu.


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichoko ameishukuru Serikali ya Watu wa China kwa kukubali ombi  lililotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Magufuli la kufadhili  wataalam wa sekta ya Afya.

Waziri Ndalichako ametoa kauli hiyo hii leo alipotembelewa na Balozi wa China nchini Tanzania Wang Ke aliyefika katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kufanya mazungumzo kuhusu utaratibu wa kupata wanafunzi watakaofaidika na ufadhili huo.

Balozi Wang Ke amesema baada ya Rais wa China kupata maombi hayo ametoa ufadhili wa Serikali yake kwa wanafunzi 20 wa Kitanzania watakaopata ufadhili wa masomo katika Sekta ya Afya kutoka Serikali ya China kwa mwaka wa masomo wa 2018/2019 katika ngazi za Uzamili na Uzamivu.

Aidha, Balozi Wang Ke amesema mbali na ufadhili huo pia Serikali ya China itaendesha Mpango wa Mafunzo kwa wataalamu wengine 20 mpaka 30 wa Sekta ya Afya kwa muda wa mwezi mmoja nchini China, hivyo amemuomba Waziri  wa Elimu kusaidia katika kuratibu upatikanaji wa Wanafunzi na aina ya mafunzo ambayo yatasaidia katika kutatua changamoto katika Sekta ya Afya.

Katika hatua nyingine Waziri  Ndalichako amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya Korea Song Geum – Young  kwa lengo la kujadili ujio wa wabunge kutoka Bunge la Korea kwa ajili ya kutoa msaada katika Hospitali ya Tiba na Taaluma ya Mlongazila.

Waziri Ndalichako amemwambia balozi huyo kuwa Serikali bado inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kujenga mbiundombinu ya kuwezesha wanafunzi na wauguzi kuishi karibu na hospitali ya Taalum na Tiba ya Mlongazila. 

Waziri amesema kwa sasa serikali ipo katika ujenzi wa awamu ya kwanza ya Miundombinu itakayowezesha wanafunzi wapatao 1500 kuishi karibu na hospitali hiyo. 

Waziri Ndalichako amesema Hospitali hiyo imejengwa kwa lengo la kuongeza udahili wa wanafunzi mpaka kufikia wanafunzi zaidi ya 10,000 hivyo bado Miundombinu itakayowezesha kuchukua idadi hiyo ya wanafunzi pamoja na watumishi wa hospitali hiyo inahitajika.

Naye Balozi wa Jamhuri ya Korea amesema serikali yake bado itaendelea kusaidia katika uendeshaji wa hospitali hiyo pamoja na miradi mingine katika Sekta ya Elimu.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Korea  Song Geum – Young ofisini kwake ambapo kwa pamoja walijadiliana namna bora ya kuisaidia uboreshaji wa Miundombinu ya Hospitali ya Tiba na Taaluma ya Mloganzila.




 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa  Joyce Ndalichako akizungumza na Balozi wa China Wang Ke kuhusu ufadhili wa masomo katika Sekta ya Afya kutoka Serikali ya China kwa mwaka wa masomo wa 2018/2019 katika ngazi za Uzamili na Uzamivu. 






Alhamisi, 22 Februari 2018

Waziri wa Elimu ashiriki kuaga mwili wa Akwilina Akwiline.


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa  Joyce Ndalichako leo ameongoza Wananchi mbalimbali kuaga mwili wa aliyekuwa Mwanafunzi wa Chuo cha Usafirishaji (NIT) marehemu Akwilina Akwiline jijini Dar es salaam.
Akizungumza wakati wa kumuaga Marehemu Akwilina Waziri Ndalichako amesema msiba huo umemgusa kila Mtanzania kwa kuwa Marehemu amekutwa na umauti akiwa anatekeleza majukumu yake ya kielimu.

Aidha, Waziri Ndalichako amezitaka Mamlaka zinazohusika kuharakisha kufanya uchungizi ili wale wote watakaobainika kuhusuika na tukio hilo waweze kuchukuliwa hatua  kwa mujibu wa  sheria za nchi.

Viongozi wengine walioshiriki kuaga mwili wa Mwanafunzi huyo ni pamoja na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Hamad  Yussuf Massauni, Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi Atashasta Nditiye , Kamanda wa kanda Maalumu ya Dar e salaam Lazaro Mambosasa  na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Leonard Akwilapo.

Mwili wa Akwilina Akwiline tayari umesafairishwa kuelekea mkoani Kilimanjaro na mazishi yanatarajiwa kufanyika kesho mkoani humo.





Jumanne, 20 Februari 2018

Waziri Prof. Ndalichako aziagiza Taasisi za Elimu kufuata Taratibu, Kanuni na Sheria za nchi


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako amezitaka Taasisi zinazotoa Elimu ya Juu hapa nchini kufuata taratibu, Sheria na kanuni za nchi katika kuendesha Taasisi hizo.

Waziri Ndalichako ametoa kauli hiyo hii leo jijini Dar es Salaam alipofanya ziara ya kushtukiza katika Chuo Kikuu cha Kampla kilichopo Gongo la Mboto  ambapo amebaini kuwepo kwa idadi kubwa ya watumishi ambao hawana vibali vya Makazi  na Ajira.
Waziri Ndalichako amesema Chuo hicho kumekuwa na udanganyifu wa taarifa za kiutumishi ambapo watu walioajiriwa kama madereva na wahudumu wamekuwa wakiingizwa katika orodha ya watumishi  ambao ni Walimu huku wakijua watumishi hao hawana sifa za kuwa Walimu.

Waziri Ndalichako amesema baadhi ya walimu katika chuo hicho kutoka nje ya nchi wanakuja kama wanafunzi lakini wakifika Chuoni hapo wanahalalishwa na kuwa walimu ambao wanafundisha wanachuo bila kuwa sifa stahiki.

Profesa Ndalichako pia amekitaka chuo hicho kuhakikisha kinafuatilia kwa karibu nidhamu ya wanafunzi wanaosoma Chuo hapo kwa kuhakikisha wanazingatia na kufuata taratibu, kanuni na sheria za nchi.

“Nidhamu ni jambo la msingi sana, sasa hakikisheni wanafunzi wanaomaliza katika chuo hiki wanakuwa na nidhamu ikiwa ni pamoja na kuzingatia kanuni na taratibu za ndani  na nje ya nchi na siyo vinginevyo, maana kuna baadhi ya wanafunzi ambao nyaraka zinaonyesha wamemaliza kwenye Chuo hiki na wako nje ya nchi lakini hawana maadili, liangalieni hili kwa umakini,”alisema Profesa Ndalichako.

Kwa upande wake  Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dk. Anna Makakala  amezitaka Taasisi zote za Elimu nchini kuhakikisha zinatoa ushirikiano kwa ofisi hiyo ili kuepuka kukiuka taratibu na miongozo iliyowekwa na nchi.